
GOSPELGTV.COM

TV ya INJILI Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM
Tel.
254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com
Back
to School But...
Anaitwa Ruth Wanjiru. Anamlilia mama asimwache Shuleni. Mpiga picha
BONIFACE MWANGI alipokuwa katika ziara ya shule za Nairobi, alimkuta
Ruth akijigaragaza chini akilia.Kwake, ni nani kama mama? Japo jina
la Shule ni GLAD TOTO NURSERY SCHOOL, ikimaanisha toto lenye furaha,
Wanjiru alionekana kutokuwa na furaha siku yake ya kwanza Shuleni
hapo. Sababu ni kwamba kuna watu walioamua kumtoa nyumbani na kumpeleka
shuleni bila matakwa yake. Haijalishi wazazi wanapenda kiasi gani
watoto wao waende shule, Lakini kama watoto wenyewe hawajui maana
ya shule, watakuwepo kuwaridhisha wazazi, na elimu ya kweli wataipata
watakapohitaji au watakapolazimishwa na hali ya maisha. Je tuwaache
watoto mpaka watakapoiona maana ya elimu ndipo tuwapeleke Shule?

Pengine Ruth anawahurumia
wazazi
Kusomesha ndio mzigo mkubwa kwa kila mzazi Kenya. Wavulana kwa wasichana
siku hizi Shule ni lazima. Utamaduni wa kuwaona wasichana wanatosheka
na urembo na siyo elimu, unaendelea kufutika kwenye mawazo ya baadhi
ya watu. Lakini asilimia kubwa ya wasichana bado wanaamini hivyo.
Lazima jitiada kubwa zifanywe kuwaelimisha wasichana wenyewe umuhimu
wa elimu. Shule za wasichana zinaongoza kwa gharama wazazi wanazolazimika
kugharamia vitu vya anasa ambavyo wasichana huona ni muhimu kuwa navyo.
Tofauti na shule za wavulana, kuelimisha msichana inagharimu zaidi,
lakini matokeo ya mitihani wasichana hufanya vizuri zaidi kwenye shule
za msingi kuliko sekondari. Wengi wanasema kwamba wakiwa sekondari
ndipo hujitambua kwamba wao ni wanawake, na huanza kufanya vitu vya
kike zaidi ya elimu. Matokeo ni kuanza kubana sketi za shule zishike
mwili kabisa, na wengine huanza kupoteza muda kujiremba badala ya
kuzingatia masomo. Hali ikiwa hivyo, hatuwezi kabisa kuwapinga mababu
waliotambua jukumu la wanawake katika jamii.Kila tunapojaribu kupingana
na maoni ya wazee wa kale, wanawake wenyewe wanafanya vitu kuonyesha
wazee walikuwa sawa.
