Ukurasa wa mbele
Soma barua Yahoo
Soma barua Hotmail

 


CNN
TBN
BBC
Times
Islamtz.org
Winners
Maranatha
Intergrity

China Today

Japan Times

Korea Online

China Site

China Maps

USA Today

Google Seach

China English

Gv China

China view

China news

China
Natinal
News

China Tech

India News

India Times

India Daily

Gospel of
Jesus

USA Gospel

Gospel
Church

Dubai news

Africa News

Gospel Music

US VISSA

BBC
Bush
Curches
Gospeltv
munishi
Mkapa
usgospel
Times
GTV
GTVGOSPEL
Jesus
God
Faith
Life
Kenya
Tanzania
Uganda
Africa
Japan
Toyota
China
Korea
India
Nation
News
Online
Nyerere
Kibaki
Museveni
Mugabe
KOFFI ANNAN
Nairobi
Dar
Goverments

gospel TV

gospelradio

Gospel radio

gospelnews

Gospel news



TV ya INJILI
Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM

Tel. 254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com


Mwinjilisti na mwimbaji wa nyimbo za Injili Jeff Njiraine Macharia anatarajiwa London. Kila kitu kiko sawa. Vissa ndiyo pekee inayosubiriwa.Kuwa na passport na barua ya mwaliko pekee hazitoshi.Bado kunatakiwa mdhamini ambaye atakubali kulipa gharama endapo mambo yataenda mrama.Hilo kwa sasa ndilo linalomsumbua Jeff.Habari kutoka London zinasema kwamba kila mwafrika London na viunga vyake anatamani kumuona Jeff.Wengine ni kwa sababu ya sanaa yake, huku wengine wakitamani kujionea yatakayojiri.Jeff anazua hisia tofauti hasa ikitiliwa maanani kwamba anaemwalika ni Nongarii. Safari ya Jeff London yaweza ikawa pigo kwa wengine.Na kuna wale watakaopata ahueni. Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili. Atakapolihubiri kama lilivyo, hatutashangaa kusikia limemrekebisha na yeye aweze kufanya uamuzi utakaowapa usingizi Mama Brenda na aliyekuwa mume wa Irene.Kwa Mungu yote yawezekana.Umaarufu wa Jeff unakaribia ule wa OBAMA. Shukrani kwa GOSPELGTV.COM Safari njema bwana NJIRAINE.
Waciama wa miujiza


Ni waimbaji wa nyimbo za Injili Kenya, Maarufu kwa jina la WACIAMA ikimaanisha wa Miujiza kwa lugha ya kikuyu. Walipowasili Moshi walikaribishwa kwa shangwe na wenyeji wao Wachagga. Walipomaliza kuhubiri pamoja na mchungaji Pius Kongo waliamua kuwatembelea waumini majumbani kama ilivyo kawaida yao. Walikaribishwa "MBEGE" kinywaji ambacho kulingana na mila na desturi za Wachagga, Mgeni rasmi lazima apewe "MBEGE" kama ilivyo kwa Waluiya wa Kenya lazima mgeni rasmi achinjiwe kuku. Waciama walisema wao wameokoka kwa hiyo hawawezi kunywa pombe. Ndipo wenyeji wao walipowasii kwamba "MBEGE" siyo pombe, bali ni sehemu ya chakula cha Wachagga kwani hutengenezwa na ndizi pamoja na ulezi. Walipouliza mbona inachacha kama pombe, waliambiwa kwamba haina tofauti na uji wapikao Wakikuyu, ambao nao huachwa uchachuke. Tena wakaambiwa kwamba walipookoka walikuwa Kenya kwa hiyo pombe walizoacha ni Tusker na Busaa za Kenya na siyo chakula kama "MBEGE" Vijana wakawa wameshawishika vya kutosha na wakajikuta wanabugia "MBEGE" Walienda kulala kwa hiyo kama ni ulevi walilewa wakiwa usingizini. Kesho yake kabla mkutano wa Injili uanze, waliona waonje "MGEGE" kidogo kabla hawajaalikwa kuimba jukwaani. Waliposimama kuimba, watu walivunjika mbavu kwa kicheko. Alianza Jeff. "Aisee Bwana. Hamjambo ndugu setu Wachagga? Tumefurahi kufika hapa Moshi japo hakutoi moshi. Tunashukuru kwa makaribisho mazuri kwani hata Mbege ya jana na leo ilikuwa tamu sana.Wakristo wa Moshi midomo ilikuwa wazi kwani wao wanajua kwamba pombe ni kileo na wale waliookoka hawapaswi kunywa. Ndipo kina Jeff na sammy walipoanza kuhubiri injili mpya kwamba wao waliokokea Kenya na Pombe walizoacha ni zile za Kenya siyo za Tanzania.

Kilichowashangaza zaidi ni kwamba kila mara walikuwa wakiapa kama Wachagga wapagani wafanyavyo. Misemo kama:"Haki ya Mungu mlima Kilimanjaro uniangukie, na mingine kama Yesu na Maria na Yoseph ilisikika mara kwa mara katika shuda zao. Mwisho waliimba lakini kwa shida kwani "MBEGE" ilikuwa inazidi kukolea akilini wakati kelele za maspika ya mkutano zilivyozidi.Mchungaji Pius Kongo alikuwa na maswali magumu ya kujibu baada ya Waciama kurudi Nairobi Kenya.Alikuwa na kibarua kigumu kufuta injili hiyo mpya kwa washirika wake ambao wengine walianza kuichapa "MBEGE" vilivyo.Wakiongea na GTV, Waciama walisema kwamba hawataisahau Moshi kwani huko walijionea mengi.Ila wanakiri kwamba pamoja na ujanja wao wa Nairobi walishindwa kuingia katika zizi la mchungaji Pius Kongo wachukue kondoo waje nazo Nairobi. Sijui walimaanisha nini hapo, Lakini hapa Nairobi vijana hao wanajulikana kwa ushapu wao wa kuwaingiza mjini mabinti.Kama hawatasema wachangiwe waoe, basi watasema wanahitaji pesa zakutoa kanda mpya ambayo haitoki.Tena kama hawatakuambia uwapatie pesa za kusafiri, basi watairudia kanda waliyokuuzia wakidai wanaenda kuimba nayo wakurudishie. Ukiwaona, basi Bikira Maria awe amekusaidia sana.Siku hizi wana mtindo mpya.Wanaenda kwenye makanisa ya Bwana Akae Nanyi, Kama wanavyoyaita.Ni makanisa yale ambayo hawakazi sana mafundisho ya WOKOVU, bali kila Jumapili Mchungaji husema Bwana awe nanyi, Na washirika Humjibu kwamba huyo Bwana hawamtaki kwa hiyo akae na Mchungaji pia. Wao wanasema wanapenda makanisa hayo kwani kila Jumapili wao ni wageni kwa moja ya makanisa hayo. Sammy naye ameamua kutumia nafasi hiyo kuwaambia wanaotaka kuolewa "NJOO TUKAE" Kwa sasa ameshawaambia mabinti zaidi ya kumi lugha hiyo na kuwaacha baada ya mizi mitatu. Aliyebahatika kuishi naye muda mrefu ni mmoja waliyekaa karibu miezi tisa. Kwa sasa macho yake yanamuelekea Penina Muimbaji wa nyimbo za Injili Meru. GTV hatuungi mkono kabisa upotovu huu. Tumekaa nao na kujadili pamoja na kujaribu kuwarekebisha bila mafanikio.Tunaona ni wajibu wetu kuwaonya waumini wajiadhari. Lakini ya Mungu ni Mengi Yanayotushinda wanadamu, Mungu anaweza kuwabadilisha.

Lakini WACIAMA wana upande mzuri wa maisha. Ni wasanii wa hali ya juu sana. Kiusanii wanaweza kufanya chochote. Itakumbukwa kwamba miaka ya 90 walivuma sana na wimbo wao "Yesu ni wa Miujiza." Japo wimbo wenyewe waliuimba kwa lugha ya Kikuyu, lakini ulivuma Afrika ya mashariki na kati. Kwa maigizo hawana mwenzao. Waliifanya serikali ya Tanzania ishindwe kupata usingizi pale walipoigiza kwamba wao ni "Wamasai watangazaji wa GTV. Walimuuliza Mkapa kama Tanzania ni yake, kisha wakasema kwamba Mkapa alivunjika miguu kwa sababu hakusikia la mkuu. Hapo walimaanisha kwamba Mkapa hakumsikia Nyerere pale alipoanza kuyauza mashirika ya umma kwa watu binafsi kinyume na siasa ya ujamaa ambayo Watanzania hawajaikana. Maigizo hayo ambayo yaliwekwa kwenye VCD yaliwafanya Polisi Tanzania wapate kibarua kigumu cha kuwakamata wote waliopatikana na VCD hizo, bila mafanikio. Hata leo vijana hao ni maarufu Tanzania na Kenya kwa maigizo yao hayo. Kwa upande wa Redio, Sammy na Jeff ni watangazaji wazuri sana hasa wanapotangaza kama "Wamasai wasijua kama hawajui. Walipoingia Dar hivi karibuni, Redio karibu zote ziliwaomba wawafanyie tangazo la kutangaza redio zao. Mpaka leo matangazo hayo huwekwa hewani na baadhi ya radio za Dar na mikoani. Redio kama Praise Power FM pamoja na WAPO FM bila kuwasahau CLOUDS FM, wote walifaidika na sanaa ya wasanii hawa matata sana kutoka Kenya. Mpaka leo Redio Biblia Husema FM ya Nairobi, wana ugomvi na wasikilizaji wao pale walipositisha kipindi alichokuwa akiongoza mmoja wa wasanii hawa. Kwa jina la kimasai SHONARA OLE TIAMBATI, Jeff alikuwa akiwavunja mbavu kwa kicheko wasikilizaji wa Biblia Husema, maarufu kama BHB.Katika kipindi cha Tufurahi katika Bwana ambacho kilikuwa kikiandaliwa katika Studio za GTV na kutayarishwa na Mkurugenzi wa GTV Pastor Faustin Munishi. Kipindi kilikuwa kikilipiwa, na senti zilipokosekana ikawa ndio mwisho wake. Lakini Redio nyingine zimekuwa zikitamani kipindi hicho kihamie kwao lakini wanapoambiwa kwamba hatuwezi kulipa kwa sasa moto wao unazimika. Waumini FM wamewahi kutusihi kipindi hicho kihamie kwao nasi tuko tayari kwa masharti kwamba Redi hiyo ndiyo itakayokigharimia kipindi. Waciama na GTV tuko tayari kutengeneza vipindi vya Redio na TV mradi tu TV na Redio husika wagharamie kipindi. Ukiwa na maoni yaandike kwenye box la maoni hapo chini.


Anaitwa Sammy Ngugi Macharia.Kucheka na kuchekesha ni kazi yake. Utathani alizaliwa afanye hivyo.Pengine ndio maana uzee unawakimbia.

Wana furaha ya asili ambayo haipatikani kwenye pesa na mali za dunia hii.Wanatosheka na kile walicho nacho.Kwao vitu siyo muhimu sana.Leo unaweza uwakute na simu ya bei ghali sana, lakini wakisikia njaa hawatajali kuiuza bei sawa na bure, mradi wapate furaha ya siku hiyo.Hawajali kama wana gari au la, hujiona huru wakiwa bila. Kile ambacho hawakosi ni jinsia ya kike karibu nao.Wakiwaona watoto kama wanavyowaita, husisimka utafikiri ni roboti zilizopigwa funguo.Usijali kama watakayokuwa wakisema ni kweli,hata wenye jinsia hiyo ni kama hupenda wadanganywe. Utawasikia wakisema wao ni watoto wa matajiri wa Kenya. Eti baba yao ndiye mmiliki wa vituo vyote vya petroli Nairobi.Hutumia hiyo kama ndoano ya kuwanasa kinadada wanaotafuta kazi. Mbinu nyingine wanayoitumia ni ile ya kusema wanaweza kuwasaidia wanaotaka kunakili nyimbo zao kwenye CD au kaseti na hata video. Hujigamba kwamba wana studio za kisasa jijini Nairobi.Mungu apishe mbali usikute hawa kinadada wa familia moja wamenasa kwenye mtego wa Sammy.

Mungu apishe mbali usikute hawa kinadada wa familia moja wamenasa kwenye mtego wa Sammy.
Kile kigumu kuelewa kuwahusu hawa jamaa, ni kwamba huwezi kujua ni wakati gani wanapomrudia Mungu na kuomba msamaha. Unaweza kuwahukumu kwa haya unayosoma hapa, ukute walitubu na kusamehewa na kurekebisha mienendo yao. Tunaomba iwe hivyo.







Huyu hapa ni Jeff akiwa na simu aliyonunuliwa na msichana wa Kenya anaefanya kazi uarabuni. Wana mipango ya kuoana.Ukweli wa mambo ni kwamba Jeff ameoa, na ana mtoto mmoja kwa jina Brenda.Haijulikani itakuwaje. Pengine Jeff ameamua kuoa wake wengi. Lakini inaonekana pesa anazotumiwa na huyu msichana aliye Saudi Arabia zinamzizua kiasi cha kuiweka ndoa yake njia panda. Mungu aingilie kati ili huyo msichana asidanganywe kuingia kwenye vita ambavyo hayuko tayari. Lakini kama akijua mambo yalivyo na bado aamue kuendeleza mahusiano yake na Jeff, basi itakuwa ni kila mmoja kuamua kusuka au kunyoa. Kwa upande wake Jeff anadai kwamba huyu mpya anaeishi Uarabuni ndiye kipenzi cha roho yake. Jitiada zetu kumpata Mama Brenda (Mke wa kwanza wa Jeff) hazikufanikiwa. Lakini tutahakikisha tumemuona ili kupata maoni yake.

Moja ya Maigizo ya Jeff na Sammy pamoja na Munishi. VCD hiyo ilizua KASHESHE la mwaka Tanzania pale Serikali ya Tanzania ilipoipiga marufuku kwa kisingizio kwamba iliikashfu CCM. GTV hatuombi msamaha kwa CCM wala Mkapa Tunasimama na maoni yetu katika VCD hiyo kwani ni haki yetu kutoa maoni.

Wengi hujiuliza kwa nini maisha ya vijana hawa ni kama maigizo? Huwezi kutofautisha wanapomaanisha na wakati wa maigizo. Mara nyingi wamekosa kuaminiwa, na hata kusingiziwa, kwa sababu ya usanii wao katika kila jambo. Mfano wanaweza wakuombe nauli ya basi kwenda mahali fulani, uwakatalie kwa sababu tu wanaigiza utajiri ambao kweli haupo.Wenyewe wanakiri kwamba wamewekwa kwenye ulinzi mkali na wake zao kwa sababu hawawaamini. Kila mmoja ameoa na wamejaliwa na watoto. Yale ambayo kila mtu alishindwa, wake zao wameyaweza. Tangu waamue kuishi na mke mmoja kwa zaidi ya miaka mitano, maisha yao yamebadilika kwa kiwango kinachowashangaza wengi.Hata wenyewe wanashangaa.Wanasema hawakuamini kwamba siku moja wangewekwa chini ya ulinzi mkali namna hiyo. Kama wanavyodai, hawakujua waliingiaje kwenye mtego na kujikuta wakiwajibika kama waume kwa wake zao. Mwanzo walianza kama utani, wakifikiri wamepata kama kawaida yao, Lakini wakawa wamepatikana. Kinachowashangaza zaidi ni kwamba wake zao hawatishi sana kwa sura, lakini mbinu za kuwamiliki wanazo.Yaani Sammy na Jeff wamemilikiwa sasa. Hawafurukuti.Na kadiri miaka inavyokwenda, na watoto kuanza kukua ndivyo wanavyozidi kunasa kwenye mtego wa kuwajibika katika jamii. Makusudi ya Mungu yanatimia maishani mwao wapende wasipende. Lakini nini kilichopelekea vijana hawa kuwa kama walivyokuwa? Wenyewe wanasema vituko vya wahubiri Nairobi viliwafanya wasitilie maanani maisha ya utakatifu kama inavyofundisha BIBLIA, na wakaishia kuona kila kitu ni kama maigizo. Wamewahi kufanya kazi ya Mungu karibu na kila mchungaji Nairobi. Kwanza walimsaidia Pius Muiru kuanzisha kanisa Nairobi, na alipopata pesa nyingi ikawa hawawezi kumuona tena. Alijiwekea walinzi wakali kuliko wale wanaomlinda rais na ikawa hawawezi kumuona. Wanasema Mambo yalikuwa mabaya zaidi wakati Muiru alipokubali kuolewa na mama wa makamo aliyekuwa akimsaidia kihuduma. Jeff anasema yeye ndiye aliyekuwa aolewe na huyo mama lakini akaruka mitego yake.Anasema bora alivyo, kuliko kuwa na kila kitu ukose utu na haki maishani.

Hata kuoa kwao kulikuwa kwa miujiza.ilikuwa hivi.Mchungaji mmoja kutoka Tanga nchini Tanzania aliwaalika kwenye mkutano wa nje. Kama kawaida yao waliamua kwenda wakiwa wamejihami kwa kila jambo. Walitafuta mabinti wawili kutoka sehemu za mashambani. Safari hii waliwapata wa kabila lao KIKUYU. Waliwaambia kwamba watasafiri kwenda Tanzania, na kwa sababu wachungaji huko huwa wanauliza maswali mengi wanapomuona muhubiri akiwa na mabinti, walikubaliana kwamba wakifika huko wasijali kutambulishwa kama wake zao. Mabinti walikubali haraka kwani ndoto zao zilikuwa kwamba siku moja waitwe hivyo. Safari ilianzia Nairobi kupitia Arusha. Walipofika Arusha iliwabidi walale siku moja. Kipesa hawakuwa sawa sana, iliwabidi wamtafute mchungaji wanayemfahamu Arusha. Walipompata walijitambulisha kama Mr.na Mrs. Mchungaji alipouliza mbona hakualikwa arusini, Jeff alidakia haraka kwamba pengine kadi ya mwaliko ilipotelea kwenye ofisi za Posta Tanzania. Alidai kwamba aliituma, na alishangaa sna kutomuona Mchungaji kwenye arusi yao iliyohudhuriwa na maelfu ya watu.Mchungaji aliguna kidogo, Lakini ilimbidi akubali japo kwa shingo upande. Alipowauliza mabinti kama kweli wote waliolewa siku moja, walionyesha kutojiamini na walipokuwa wakijitizama kwa haya, Sammy aliingilia kati na kusema bado wanaona haya kwa sababu masuala ya kuolewa ni mageni sana kwao. Alisisitiza kwamba kama siyo UTUMISHI WA MUNGU, saa hizi wangekuwa kwenye hoteli moja ya kifahari jijini Nairobi wakiendelea na 'HUNEY MOON yao. Mchungaji alionyesha kuwahurumia, na akawatafutia kila mmoja chumba chake ili kila mtu awe na wakati wa faragha na "mke wake" Pia alihakikisha kwamba amewapa shuka mpya ili malazi yawe matakatifu. Laiti angejua kwamba ndiye anayeibariki ndoa yao kwa mara ya kwanza. Baada ya chakula cha jioni, Mchungaji aliongoza maombi na kuwaruhusu wakajipumzishe. Kwenye maombi yake Mchungaji aliomba hivi. "Mungu Baba tunakushukuru kwa ajili ya wageni. Tuliwajua walipokuwa vijana, na imekupendeza kwamba umewapa wasaidizi watu wa kufanana nao. Ni wewe uliyesema kwamba mtu atamuacha baba yake na mama ili aambatane na mke au mumewe. Tizama watumishi wako hawa kutoka Kenya ambao hawakuona kuoana pamoja na raha zake ni kitu cha dhamana kuliko neno lako, na ndiyo maana wakiwa katika siku zao za mwanzo wa ndoa, wameamua kuja kuifanya kazi yako nchini Tanzania.. Eee Bwana bariki usingizi wao katika nyumba yetu, na Kesho wanapoendelea na safari yao mjini Tanga utawabariki na pia utaubariki mkutano watakaokuwa nao huko. Tunasema asante maana tumeomba machache hayo katika Jina la Yesu Kristo aliye Bwana na Mwokozi wetu." Na wote waliitikia AMEN.

Mchungaji bila kujua, alikuwa amewaoza watu kwa mara ya kwanza. Hata wewe unajua kilichoendelea. Siyo lazima niseme.

Asubuhi baada ya kupata kifungua kinywa, mchungaji wa Arusha ilibidi awasaidie "Watumishi wa Mungu" nauli ya kuwafikisha Tanga, pamoja na pesa kidogo za matumizi njiani. Njiani walikuwa wakicheka, Kinadada nao soni zikaanza kuwaisha usoni. Pengine walianza kufurahia kuitwa"wake." Kufika Tanga walipokelewa kwa shangwe na wimbo ukawa ni ule ule. Baada ya mkutano kwisha, Kinadada wa Tanga walionekana kupenda sana kuwa karibu na "wake wa watumishi wa Mungu Toka Kenya" Maswali waliyokuwa nayo kuwahusu wasanii hawa machachari waliyaelekeza kwa "wake zao",Jambo ambalo halikuwapendeza sana Jeff na Sammy. Uongo walioutunga wenyewe, ukaanza kuwaendea kinyume. Waliwatamani sana mabinti wa Tanga, lakini "WAKE BANDIA " wakaanza ulinzi wa kweli. Kila walipojaribu kuutafuta mwanya wa kuwaacha kidogo Hawa wake waliwaganda kama kupe amgandavyo ngombe. Mbaya zaidi walikuwa wamewafundisha mbinu za kudanganya wakati wa matatizo. Ikwa wake Bandia wamepata nafasi ya kuwajua ndani na nje na ikawa ni vigumu sana kudanganywa. Baada ya mkutano wa Tanga, kile walichofikiria ni kupata, kikawapata. Mkutano wote ulitangaziwa kwamba Jeff ameoa, na pia Sammy ameoa. Hayawi hayawi mwisho yakawa. Waliondoka Tanga Mate yakiwatiririka kwa tamaa, kwani kama wanavyosema wenyewe, watoto huko ni kama wakuchongwa siyo kuzaliwa. Tena wanadai kwamba wana heshima gunia zima kama siyo debe zima. Siyo kwamba wanawadharau wake zao, Lakini wanakiri kwamba waliwapata haraka kwa ajili ya safari na haikuwa ule uchaguzi wao hasa. Walikuwa wamejiwekea viwango ambavyo wanakiri kwamba wake zao hawana. Pengine Mungu aliyaona mateso ya mabinti waliodanganywa kwamba wangeolewa na wasanii hawa bila mafanikio, na akaamua kuwaoza kilazima, au kama wanavyosema Kenya, Waliozwa KYANGUVU. Waliporudi Nairobi walijaribu kila mbinu wajinasue wabaki huru, Lakini watoto wa KIKIKUYU walikuwa na mbinu mmbadala. Waliwashinda maarifa mpaka wote wakapata watoto na wakawalazimisha kwenda kwa wazazi wao na sasa ni miaka zaidi ya mitano, na kama bado wana ndoto za kuoa wasahau kwani urefu wa maji waliyoyaingia ni vigumu sasa kutoka. Inaonekana kwamba wameikubali hali hata kama ni shingo upande. Umri nao umeanza kuwapiga chenga kwani sasa hawawezi kumdanganya binti yeyote kwamba wao ni vijana wa tajiri fulani Nairobi. Vijana gani ambao kichwani nyele zina mvi moja moja? na kila kukicha zinazidi kuongezeka. Isitoshe watoto wanakua. Tena wake zao sasa wanazijua mbinu zao zote. GTV tunamshukuru Mungu aliyewatumia mabinti jasiri wa KIKIKUYU kumaliza kile kilichoonekana kama tishio la kazi ya Mungu Afrika ya mashariki. Shetani akiwatumia vijana hao wakati wa ujana wao, wakijua au bila kujua, walikuwa wameharibu sana USHUHUDA wa Yesu Nairobi na kote walikowahi kutembelea vijana hao ambao sasa ni wazee wanaoelekea uzeeni. ILa hata sasa wanasema hawakosekani wanaotaka kujua wenzao walikuwa wakidanganywaje? Ushauri wetu kwao ni kwamba wala wasiulize. Isije ikawa wanaamsha maroho yaliyolala kuzimu yaje tena yaanze vituko. Tunawaombea Mungu awape nguvu ili wakati huu uliobaki maishani mwao wautumie kuliinua Jina la Yesu ambaye walikuwa wakimrudisha msalabani kwa matendo yao. Pia waitumie nafasi hiyo kuwakemea wachungaji bandia ambao wanatumia maroho ya kuzimu kufanya kile kinachoonekana siku hizi kama miujiza. Eti watu watoe pesa wampe mchungaji, naye awamwagie mafuta ya karanga usoni kama baraka. Huo ni uongo kutoka kwa shetani mwenyewe na tunaukemea kwa jina la Yesu USHINDWE. Kabla hujaanza kuwahukumu soma kisa kifuatacho halafu ujaze mwenyewe.

James Kim Apokonywa mchumba

Baada ya kujitafutia mchumba, walipanga siku ya kufunga pingu za maisha. Kabla ya kujuana kimwili, James alimuona mchumba wake akiwa na mimba. Tofauti na ile ya bikira Maria iliyokuwa kwa uwezo wa roho Mtakatifu, Hii ya mchumba wa James ilikuwa kwa uwezo wa Pastor "MWENYE ROHO MTAKAVITU". Pamoja na jitihada za Pastor huyo kumtaka Kim amuoe msichana huyo, inasemekana kwamba juhudi hizo zimegonga mwamba kwani James Kim amekataa kata kata.Ndoano iliyotumika kumnasa binti huyo ni "Huyo Kim ana nini? Tafuta nyumba Buru Buru na kama unataka sana kumuona huyo Kim wako, basi nitamwajiri awe mlinzi wa usiku kwenye hiyo nyumba" Hayo ndiyo maneno yaliyommaliza nguvu mchumba wa Kim. Na kweli inasadikiwa kwamba msichana huyo amekodishiwa nyumba kwenye mtaa wa Buru Buru mjini Nairobi, Lakini kim ameikataa kazi ya WATCHMAN huko. Mengi zaidi muulize James kim Mwenyewe kwenye simu ya mkononi +254723552655

Kanda Mpya

Mwinjilisti James Kim amechomoa kanda mpya. James aliyekuwa mchezaji hodari wa vyombo katika huduma ya Mchungaji James Maina Nganga. Inasemekana kanda yake hiyo, imeanza kupata umaarufu katika Kanisa la Neno Evangelisim. Muda mfupi baada ya kanda hiyo kutoka, uhusiano wake na Pastor ulianza kuzorota, jambo lililopelekea kusimamishwa huduma mara moja. Kwa sasa hana masoko ya kuiuza kanda yake kwani alitegemea kanisani ambako alihudumu kungekuwa soko la kwanza kabla ya wengine kuijua kanda yake. Akiwa katika Ofisi za Gospel GTV, alituonyesha barua aliyopewa kusitisha huduma yake kanisani hapo.


Inaonekana kuna vita baridi kati ya waimbaji na wachungaji. Wachungaji wakiona huduma za waimbaji zinaaza kushamiri, wanaanza mbinu za kuwamaliza kihuduma. Hatuungi mkono utovu wa nidhamu kati ya baadhi ya waimbaji, Pia sambamba na hilo, Hatuwaungi mkono Wachungaji wenye wivu. Matatizo ya waimbaji mengi wamejiletea wenyewe, Lakini ni kweli kwamba wachungaji nao wanachangia pakubwa kuwadidimiza waimbaji. Katika ukurasa huu kumejaa visa vya waimbaji walioteswa mikononi mwa wachungaji wenye wivu na wengine tabia zao haziambatani kabisa na maandiko matakatifu. Hii imeendelea kujenga ukuta mkubwa kati ya waimbaji na Wachungaji. Hakuna sababu ya Mchungaji kuwasakama Waimbaji kwa sababu tu wametoa kanda ili wajitegemee. Kuna ubaya gani kufanya hivyo? Waimbaji wengi hufanya huduma zao makanisani kwa misingi ya kujitolea na siyo vibaya wakijikwamua kiuchumi wakitumia sanaa yao.Wengi hawalipwi, na kama wanalipwa ni kidogo sana kuwawezesha kumudu mahitaji ya kila siku. Kuwatumia waimbaji halafu uwatupe unapofanikiwa kihuduma, ni sawa na kuwaua. Hiyo haimpendezi Mungu hata kidogo.Mapato ya makanisa mengi huishia mifukoni mwa wachungaji wakati waimbaji huambiwa wamtumikie Mungu. Kwani kuna kosa gani kwa muimbaji kumtumikia Mungu huku akitumia sanaa yake kujilisha na kujivisha? Je Wachungaji wanapotumia vibaya pesa za kanisa kwa anasa, Nani awape barua ya kuachishwa kazi? Wengine hudai kwamba wao wameitwa na Mungu kwa hiyo wana haki ya kutumia pesa za kanisa wapendavyo. Siyo kweli.Kanisa ni washirika pamoja na Pastor. Bila washirika kusingekuwepo na pesa ambazo Wachungaji hujivuna nazo

Redio za Injili na Wanamuziki wa Gospel
.
Mwinjilisti Kim akifikiri kazi imeisha, Alijikuta ndio kibarua kinaanza. Alirauka asubuhi kuanza kuzitembelea Redio Stesheni ili ziweze angaa kucheza nyimbo zake ziweze kujulikana. Hakuyaamini masikio yake pale alipoambiwa wazi kwamba lazima atoe kitu ndipo nyimbo zake ziweze kusikika. Kwa kijana ambaye ameachishwa kazi na kupewa Elfu tano ambazo alilipia nyumba zote, kumwambia atoe pesa ndipo nyimbo zake ziwekwe hewani , ni sawa na kumtuma James Kim maziwa ya kuku na sijui atayapata wapi. Baada ya kutoka KBC ambako walichukua CD yake bila kuahidi wataicheza lini, Kim alienda Redio CITIZEN ambako nao pia walimpokea vizuri na kuichukua CD yake. Lakini alipofika kwenye redio ya Injili BHB ambako alitegemea kukaribishwa vizuri kuliko alikotoka, Huko Biblia husema aliambiwa lazima alipe shilingi elfu mbili ndipo nyimbo zake zichezwe. Alipouliza kama atapewa risiti ya pesa hizo isiwe kwamba anatoa rushwa, Alijibiwa kwamba risiti ataipata. Ilimbidi Kim azunguke mguu na njia ili kuweza kupata Kshs.2000. Mungu alikuwa mwema kwake kwani msamaria mwema aliamua kumsaidia baada ya kuelezewa magumu aliyopitia Kim. Alirudi haraka BHB na kuwalipa, na siku hiyo hiyo walianza kuucheza wimbo wake ambao kila anayeusikia anabarikiwa rohoni. Kweli safari ya WOKOVU ina mengi njiani.
Hapa ni risiti Kim aliyopewa BHB baada ya kukataliwa katakata kwamba nyimbo zake haziwezi kuchezwa bure.

Mwinjilisti James Kimwele.
Mungu akikugusa kumsaidia kijana huyu, Fanya hivyo kwa kutumia simu yake +254723552655 Ni mchezaji mzuri wa gitaa, na karibu nyimbo zote alizowahi kuimba mchungaji Nganga kijana huyu ndiye hucharaza Lead Gitaa au Bass.Pia anajua kucheza piano vizuri sana.



Huduma ya NENO
Kwenye Internet

http://nenosasa.netfirms.com

Tel. 254722410381 E-mail:
jamainga@yahoo.com
Huduma ya Neno sasa yatinga Nairobi
Mchungaji James Maina Ng'ang'a sasa ametua Nairobi. Kile alichokitamani siku nyingi sasa kimetimia. Mwenyewe anadai ni wakati wa Mungu umefika awe na huduma kubwa Nairobi, na hakuna mtu wala shetani atakayezuia hilo. Akizungumza kuhusu ajali mbaya aliyoipata karibuni, alisema amejua kwamba zilikuwa mbinu za shetani kumzuia asiingie Nairobi kwa kishindo. Kanisa lake liko barabara ya uhuru karibu kabisa na mahali lilipo kanisa la Redeemed ambalo linasimamiwa na Mchungaji Wilfred Lai. Sijui ilikuwaje, lakini hata Mombasa makanisa ya hawa wachungaji wawili huwa yamekaribiana kiasi cha kuwafanya watu waamini kwamba wanashindana. Lakini Ng'ang'a alisema kwamba yeye hashindani na Mtu bali anayeshindana naye ni Shetani. Kwamba imetokea kupata kiwanja jirani na kanisa jingine hiyo haina maana kwamba kuna ushindani wowote. Aliwahurumia wanaodhani kwamba yeye anashindana nao. Alisisitiza kwamba ni mawazo hayo potovu ndiyo yanayowafanya wengine wampige vita ambayo yeye hajajiandaa kupambana. Alimaliza kwa kusema wanajisumbua, na hawatafaulu kwani Mungu ameamua kumwandalia meza machoni pa watesi wake.


Serikali Kenya Darubini kwa Ng'ang'a

Kushoto ni Pastor James Maina Ng'ang'a, wakiwa na kiongozi wa kundi la MUNGIKI.
Mchungaji Maina Nganga alianzia Mombasa na sasa yuko Nairobi. Kanisa la Mombasa limefifia huku washirika wakihamia makanisa mengine. Aliyefaidi sana Mombasa ni mchungaji Panga ambaye washirika wengi wa Nganga wamehamia kwake. MTAKA YOTE HUKOSA YOTE ndivyo wanavyosema Mombasa. Wengine wanasema TAMAA ILIMPONZA FISI. Naye mchungaji Nganga anasema sasa Mungu amemwita Nairobi, na Mombasa ikae.

Nayo serikali ya Kenya imekuwa ikimfuatilia kwa karibu mchungaji Ng'ang'a baada ya kiongozi wa kundi la Mungiki kudai ameokoka na kujiunga na kanisa la Ng'ang'a. Wanaiona hiyo kama mbinu ya MUNGIKI kuja na sura mpya ya kanisa la Neno Evangelism.

Wanaomsaidia kihuduma wanalipwa pesa kidogo sana na hazitoshi kumudu mahitaji yao. Wengi wamehamia katika kanisa la Mchungaji Lai Mombasa kwani anawalipa mara tatu ya wanavyolipwa NENO. Wahudumu wa NENO wengi hulipwa Kshs. 5000 kwa mwezi. Wanapohamia kwa LAI wanalipwa mara tatu ya walivyokuwa wakipokea walipokuwa kwa Ng'an'ga. Japo kila siku sadaka hutolewa zaidi ya Kshs.100,000 lakini kutokana na matumizi mengi mchungaji bado anadai hazitoshi. Maisha ya kifahari, miradi mingi isiyomalizika, imefananishwa na mtu aliyeweka unga kabla maji hayajachemka na anajaribu kusonga ugali. Haijalishi ataongeza moto kiasi gani, lakini ugali huo hauwezi kuiva.

Wengine wanamlaumu mchungaji Ng'ang'a kwa kujitakia makuu. Wengi wa washirika wake wanalalamika kwamba matumizi katika kanisa hilo ni ya juu kiasi kwamba hawawezi kuyamudu. Walitoa mfano wa vipindi katika redio na TV. Bei zake ni juu sana kwani kila wiki wanalazimika kulipa KSHS. 70,000 hiyo ni kwa ajili ya vipindi katika vyombo vya habari tu. Pia walisema kila mwezi hulazimika kulipia nyumba ya Mchungaji huko Nyali Mombasa na nyingine Runda Nairobi. Nyumba ya Mombasa ni KSHS 30,000 kila mwezi wakati ile ya Nairobi ni KSHS 40,000 kila mwezi. Walikumbusha kwamba nyumba hizo lazima zilipiwe miezi mitatu mbele.

Tena walilalamika kuhusu michango ya kununua gari la mchungaji. Kwa imani mchungaji hupenda kuendesha gari kubwa ya kifahari na ya kisasa kabisa. Kwa sababu kampuni za magari hutoa magari kila kukicha, hakuna siku watamaliza kununua gari la mchungaji. Likitoka jipya mchungaji anasema ataliendesha kwa imani. Imani ya mchungaji inawalazimu washirika waingie mifukoni kuitimiza imani hiyo.

Wengi waliokuwa wakuu katika mashirika imewabidi wafutwe kazi baada ya mashirika hayo kupata hasara ya mamilioni ya pesa. Kuna wale wanaosema hasara kwenye mashirika hayo ilisababishwa na ufujaji wa pesa zilizopelekwa kanisani kulipia gharama za juu kanisani ambazo hakuna dalili kwamba zitamalizika karibuni. Ni kweli kila mtu amepewa huduma tofauti na mwingine, lakini tofauti hiyo ikiwa ni kuwalemea washirika na mahitaji ya pesa yasiyoisha, tuna mashaka kama na hiyo ni huduma ya Mungu.


Siyo kweli kwamba wahubiri ni watu waliokosa la kufanya.
Mchungaji James Maina Nganga alikuwa na mengi ya kufanya kabla hajaanza kuhubiri. Alipotoka jela alianza kuuza kaseti za nyimbo za injili akitumia baiskeli.


Mchungaji James Maina Nganga, tayari kikazi.


Pasror Mr. and Mrs. James Maina Nganga
"Haki za wanawake ni kubaki wanawake, wakati haki za wanaume ni kudumu wanaume. Wanawake hawawezi ya wanaume, pia wanaume hawawezi ya wanawake. Mashindano ya nini kati ya wanawake na wanaume? Kwa nini wanawake wanatamani kuwa wanaume?"




Pastor James Maina N'gan'ga.
"UPAKO huleta mali, lakini mali haiwezi kuleta UPAKO." Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.


Mchungaji Maina akiwa na gari yake ya kifahari kabla haijapata ajali.


Huwezi kuamini baada ya ajali hii mbaya Mchungaji Ng'ang'a alitoka bila majeraha yeyote. huo ni muujiza wa Mungu kwa mtumishi wake. Mwenyewe amekuwa akihubiri kwamba hatawahi pata ajali maishani mwake. Pengine ajali hii ni fundisho kwake na kwetu pia. Mungu asifiwe. Kwa sasa Kanisa la NENO Nairobi linakita mizizi jambo linalozua upinzani mkubwa kutoka hata kwa wachungaji marafiki zake. Kitonga aliyekuwa rafiki wa karibu, sasa i8nasemekana ndiye anayepinga kwa nguvu zote kanisa la NENO kujengwa karibu na NGOME yake Nairobi.

Washirika Nairobi wa nani?

Nairobi washirika ni sawa na Kondoo waliokosa Mchungaji. Walitoka kwa Mchungaji Mwarandu wakajiunga na Pius Muiru. Sijui waliona nini kwa Muiru, wakahama kwenda kwa James Maina Nganga. Sasa Pastor Nganga anawatingishia funguo za Benzi aliyonunua kwa pesa zao. Nasikia kwamba hata kwa Nganga hawakai. Safari hii sijui wanataka kuhamia kwa nani? Muiru ambaye alikuwa akitamba kuiteka Nairobi na Injili, amejikuta bila wathamini baada ya kundi kubwa la matajiri kulihama kanisa lake. Hata mbinu za kuhubiri imembidi abadilishe. Badala ya mahubiri watu waliomzoea kwayo, sasa Muiru anatabiri kama mganga wa kienyeji. Anakaa mbele ya Camera ofisini kwake, na kuanza kutaja mambo ambayo ni kawaida na ni lazima apatikane mwenye matatizo anayoyatabiri. Mfano akisema kwamba kuna mtu mwanamke mwenye matatizo ya kizazi, na Mungu atamponya kama atatoa shilingi elfu tatu kusaidia huduma ya NURU GIZANI, Lazima watatokea wanawake wengi wenye matatizo kama hayo. Kinachowasumbua wengi akili ni kama baada ya kutoa pesa hizo kweli watapona?

Kundi linalowafadhili wahubiri si watu wengi. Wakiamua kuhama itakuwa vigumu kwa wahubiri kumudu gharama za juu kuendeshea huduma zao.Inasemekana kwamba wahubiri wanaoonekana kwenye TV gharama zao ni Kshs.500,000 kwa juma moja. Sasa matajiri wazito wakihama kama walivyomhama Muiru, Sishangai kumsikia akisema kwenye TV kwamba Bwana amemwonyesha kwamba yule mtu ambaye kanisa limejengwa kwenye shamba lake, asarende hati za kumiliki shamba hilo kwake mara moja, kwani hiyo ni amri kutoka juu kwa Mungu mwenyewe. Wengi walishitushwa na kauli hiyo na wakabaki wakijiuliza nini kitafuatia baada ya kusarenda hati za kumiliki mashamba? Pengine kitakachofuata ni kusarenda wake zetu kwa wahubiri. Mungu asaidie tusifike hapo, lakini kila dalili zinaonyesha tunaelekea hapo. Maisha ya hali ya juu yamewalewesha wahubiri na hawataki kushuka. Lakini Mungu atawashusha.

Wengine wamefikia hatua ya kujitengenezea kile watakachokiita miujiza kwenye TV. Wanachaguliwa watu watakaosema kwamba wamepona ili kuvuta umati kanisani. Wakija wasipone, wanaondoka kimya kimya. Kwa sababu TV bado inatumika kuwatapeli, kila siku hawakosi watu wapya. Wanakamuliwa, wakikauka wataondoka wapishe wengine. Yaani mtindo wa makanisa umegeuzwa na kuwa kama gari la abiria. Linabeba likishusha na hakuna abiria wanaoweza kusema gari ni lao. Makanisa nayo hivyo hivyo yamekuwa ni mali ya wachungaji na familia zao. Washirika hawana lao. Wanachopata ni mafundisho yenye chumvi nyingi, ikiwashinda kumeza, wanaambiwa wameze kwa lazima ya Mungu. Wanatoa na hawaruhusiwi kuuliza pesa hizo zinatumika vipi. Yani Kanisa ni kama KIOSK ya Mchungaji. Anafungua KIOSK asubuhi saa kumi na mbili. Wanaingia kwa maombi ya asubuhi, maarufu kama "Morning Glory" Sadaka asubuhi lazima watoe. Mchana wanakuja maombi ya mchana maarufu kama "Lunch Time Meeting" Hapo pia wataahidiwa ahadi za baraka kutoka kwa Mungu, lakini wao wanapaswa kumbariki Mchungaji wao anunue BENZ ya milioni kumi na tano. Jioni bado watakuja kuombewa baraka pamoja na kupakwa mafuta, kisha wataulizwa kutoa ili kiwanja cha kanisa kinunuliwe. Bei ya kiwanja wataambiwa ni milioni 30 pesa za Kenya. Kila mtu atatoa mpaka akose nauli ya matatu kurudi wanakoishi. Usijali kama kweli kuna kiwanja kinachonunuliwa, au pesa hizo zinatumika kujenga nyumba ya kibinafsi ya mchungaji katika mtaa wa Karen, na hata kama kiwanja kikinunuliwa, na tuna mashaka kama kitanunuliwa, kitakuwa kimesajiliwa kwa jina la mchungaji na siyo Kanisa. Hata washirika wakiamua kumtimua Mchungaji, Hawawezi kulipa madeni ya mamilioni ya shilingi kanisa linayodaiwa na vyombo vya habari ambavyo hurusha vipindi vya mchungaji huyo. Watajiuliza mbona tunachangishwa kila siku kulipia vipindi? Kumbe kwa makusudi Mchungaji halipii vipindi hivyo ili kuwazuia washirika wasije wakawaza kumtimua wachukue usukani Kanisani hapo. Kwa Mchungaji mkimtimua atachukua mkoba wake aondoke awaachie kiwanja ambacho siyo mali yenu, Tena hakuna dalili zozote kuonyesha kwamba kiwanja husika kinatarajiwa kuwa mali ya kanisa, Nadhani wengi watazimia kuambiwa kwamba kiwanja hicho hakijalipiwa chochote. NI ugumu huo ndio unaowafanya washirika wakose nguvu ya kudai haki zao. Nasi tunauliza. Mpaka lini wahubiri matapeli wataruhusiwa kuwaibia watu mchana machoni pa Serikali na kila mtu?

Wamasai wanaohubiri kwenye Redio Biblia Husema maarufu kama Shonara Ole Tiambati na Samiet Ole Leteipan wameigiza kipindi "Hakuna nuru gizani" Bonyeza hapa chini usikize kipindi.
MASAI: Hakuna Nuru Gizani!!

Serikali Kenya yatishia kubomoa Kanisa

Wanasema Kanisa pamoja na majengo mengine yako barabarani na ni lazima yabomolewe. Ni amri ya serikali. Tunaomba iwe siyo kulipiza kisasi. Mke wa Muiru alikuwa na bado ni kipenzi cha chama kilichotolewa madarakani KANU. Wakati wengine walilipa kutumia ukumbi wa KICC, Yeye alipewa bure kuutumia ukumbi huo apendavyo. Hata kama alilipa basi ilikuwa sawa na bure.

Lakini hii haiwapi haki serikali ya sasa kulibomoa kanisa la MAXMAM MIRACLE CENTRE. Pamoja na kwamba Muiru amekiri kutokuwa na hati ya kumiliki eneo lilipojengwa kanisa, kama walipata kihalali hakuna mwenye haki ya kuwanyanganya kwa kisingizio cha barabara. Picha inaonyesha wazi kwamba barabara ziko mbili na kuna nafasi kubwa katikati na pembeni kuiongeza barabara husika bila kuharibu mali za raia na hasa makanisa ambayo ni mahali pa kumwabudu Mungu.

Dunia na Vyote ni mali ya Mungu.

Inashangaza kuona kwamba ili wahubiri wapatiwe sehemu za kujenga makanisa, lazima wajipendekeze kwa wanasiasa. Tatizo ni wakati wanasiasa wanapotolewa madarakani na wengine kuingia. Dunia ya Mungu chini ya sheria za wanasiasa. Mpaka lini tutaendelea kunyanyaswa kwenye dunia ya muumba wetu? Hivi kweli sehemu za kuabudia zinaweza adimika kiasi ni lazima tuwapigie magoti wanasiasa? Wao waliumba dunia gani mpaka kibali cha kujenga mahali pa kuabudia watoe wao?

Hatupingani nao, ila wafanye waonavyo ni vyema. Lakini wajue Mungu mwenye dunia na kila kitu mpaka maisha yao anawatizama. Hawawezi kutudanganya kwamba tuna UHURU wa KUABUDU wakati kupata sehemu ya kuabudia ni kitendawili. Sheria hutungwa na watu kwa ajili ya watu. Sheria zinapotumika kuwabomolea watu mali zao, ni wakati wa watu kutunga sheria nyingine za kuwajengea watu mali zao. Amri za Mungu hazibadiliki kwani hazina makosa. Sheria za wanadamu zinatakiwa zibadilishwe kila mara kwani wanadamu wana makosa mengi. Nini kinachowafanya mfikiri kwamba sheria za sasa hazina makosa?

KWAMBA TAFSIRI YA SHERIA INAWEZA PINDISHWA ILI IWAADHIBU WANAOTAKIWA KUADHIBIWA NAYO HILO NDILO LINALOTUPA MASHAKA. JE! NIA YA SERIKALI NI KWELI KULINDA SHERIA NA UTENGAMANO AU KUWATAFUTA WALIOIUNGA MKONO SERIKALI YA AWALI ILI WAADHIBIWE. SERIKALI YA SASA INATAKA KUUNGWA MKONO. JE INATAKA WANAOWAUNGA MKONO SASA NAO WAJE WAADHIBIWE NA SERIKALI IJAYO? AU WATATAWALA MILELE? KILA LA KHERI.

Pastor Pius Muiru Wahubiri wanampiga vita, na sasa SERIKALI? Lazima tusimame na Mtumishi huyu wa Mungu wakati huu wa mateso kutoka SERIKALINI. Wanasema ukiona mwenzako ananyolewa kichwa tayarisha. Hujui zamu yako ni lini. Hata kama Rais ni MKATOLIKI, hatuwezi kulazimishwa wote tuwe wakatoliki. Haiwezekani.


Tangaza Biashara yako Bure
Tuma picha na maelezo kwa munishi@munishi.com

http://munishi.com
FREE!

Send photo and information to munishi@munishi.com


Redio Injili FM
Sasa unaweza kuisikiliza Redio INJILI FM OnLine. Bonyeza Hapa

Wimbo mpya CCM imewatesa wengi
Wanahabari Wanafiki
MASAI: Hakuna Nuru Gizani!!
Hotuba ya Munishi kwa TAIFA


Redio Injili FM

Sasa unaweza kuisikiliza Redio INJILI FM OnLine. Bonyeza Hapa

Hii ni redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Yesu ni nuru ya ulimwengu, Alikuja tutoke gizani. Giza na nuru hazikai pamoja. Yaani hakuna nuru gizani. Mungu anakupenda jinsi ulivyo. Ukimwamini na kutubu makosa yako utaokoka. Huwezi kuokoka ndipo uamini baadae. Hapana. Kwanza unaamini, kisha unatubu, na ndipo Mungu anakusamehe na kukupa uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu. Uwezo wa Mungu ndani yako ndio wokovu. Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com

Ukisha pokea msamaha wa dhambi, omba lolote kwa Mungu na maombi yako yatajibiwa. Katikati yako na Mungu ni Yesu peke yake. Siyo Mchungaji wala Askofu. Omba mwenyewe kwa jina la Yesu, na Mungu atakujibu maombi yako. Baraka za Mungu hazinunuliwi kwa pesa. Huwezi kumhonga Mungu ndipo akubariki. Mungu ni tegemeo letu sote. Wachungaji na washirika, tunatakiwa kumtegemea Mungu kwa baraka zetu. Siyo wachungaji wawategemee washirika kwa baraka zao, huku wakiwaambia washirika wamtegemee Mungu. Nani walio katika nafasi nzuri zaidi kumtegemea Mungu? Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com

Je baraka za Mungu zinawezaje kumpita mchungaji ziwaendee washirika ili washirika wambariki mchungaji? Siku hizi washirika wanawinda baraka zao kutoka kwa wachungaji, Wanasahau kwamba hata wachungaji wanawinda baraka zao kutoka kwa washirika. Wanajiunga na makanisa yaliyovuma ambayo wachungaji wake wanatembelea magari makubwa na kuishi kwenye mitaa ya kifahari. Lengo ni ili na wao wafanikiwe kimaisha. Wakifika wanashangaa kukuta mchungaji anawategemea ili wayalipie maisha yake ya kifahari. Walienda kutafuta mafanikio, wanarudi wakiwa masikini kuliko walivyokuwa. Walikosea lengo. Tunatakiwa kumtafuta Mungu kwanza, na hayo mengine tutazidishiwa. Hiyo ndiyo INJILI. Jiunge na kanisa kwa lengo la kuutafuta uhusiano wako na Mungu. Usijali kama kanisa hilo lina watu wengi au la. Nani alikudanganya kwamba wengi hawawezi kuwa wamepotea njia? Jiunge na wale wanaomtafuta Mungu kwa moyo wao wote hata kama ni wachache. Sikiliza sauti yake

UPONYAJI

Unaisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Hujambo msikilizaji. Tunamshukuru Mungu kwa ulinzi wake maishani mwetu. Ndiyo maana tunamtukuza na kumwabudu siku zote. Shetani ni muongo. Lazima tupambane naye kila iitwapo leo. Anatumia kila mbinu kuwapotosha watu wa Mungu, Lakini Bwana Yesu asifiwe kwani tumezigundua hila zake. Alifikiri akiwatumia wale wanaojiita wahubiri hatutamgundua. Alijidanganya. Tunajua kwamba yeye huweza kujigeuza na kuwa kama malaika wa nuru. Hatujali atatumia nani, lakini tukiziona dalili zake popote na kwa yeyote tutamkemea arudi kuzimu. Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com

Kifo cha Yesu msalabani na hatimaye kufufuka siku ya tatu kilimaanisha mengi kwetu tunaomwamini. Sasa tunapokea msamaha wa dhambi, Wokovu wa roho, Uponyaji wa mwili, na baraka maishani Bure. Mtu asikufanyie sarakasi, mbembwe, vitimbi, eti akusukume uanguke ndipo upokee uponyaji. Injili ya Yesu inasimamisha haiangushi. Shetani kazi yake ni kuangusha kwani mwenyewe alianguka kitambo. Ukiona mahali watu wanaombewa na kuanguka anguka hovyo ujue shetani ana mkono wake hapo. Kama nguvu za Mungu ndizo zinazowaangusha, mbona mhubiri huwa haanguki? Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com

Wengine wanasema wanafanya miujiza kumpita Yesu. Sawa. Je kiutakatifu pia wamempita Yesu? Nina mashaka kama hata wanamkaribia.Hii ni mbinu ya shetani kuongeza chumvi kwenye injili. Tunaikemea katika jina la Yesu ishindwe. Ndiyo ninaamini kwamba Yesu anaponya. Tatizo langu ni watu wanaotumia uponyaji wa Mungu kujinufaisha kibinafsi. Mungu ndiye anayeponya na siyo mhubiri. Uponyaji wako unategeme Mungu na wewe kuliko mhubiri. Hata kama ana nguvu za kuangusha watu, na pengine siyo nguvu za Mungu, haina maana kwamba wewe utapona kwa kuitumia imani yake. Haiwezekani. Kama hujaisikia injili vya kutosha imani yako ijengeke, hata ukiangushwa mara ngapi. Haitaleta tofauti yeyote. Utaangushwa uanguke, ukiamka utakuwa umepoteza pochi na viatu, lakini bado utakuwa mgojwa kuliko mwanzo. Ukimuuliza huyo mhubiri wa vituko, mbona hujapona, utaambiwa kwamba hujatoa fungu la kumi. Utauza gari na shamba ulete pesa zote kwa mhubiri huyo tapeli, lakini bado hali yako itazidi kuwa mbaya. Ni mpaka uijue kweli ya Injili ndipo utawekwa huru. Kweli inasema kwamba kwa kupigwa kwa Yesu wewe ni mzima. Siyo kwa kuangushwa chini. Pole sana. Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com

Yesu katika mahubiri yake hakufanya maonyesho tunayoyaona na wahubiri leo. Alihubiri na kufundisha kweli ya Mungu, walioamini walimwendea ili awaponye, aliwaambia wapokee kadiri ya imani zao.Yesu hakuwahi kuwaombea wagonjwa wakakosa kupokea uponyaji wao. Tena Yesu hakutumia imani yake kuwaponya wagonjwa. Kila mara aliwauliza waliomwendea kama wanaamini anaweza kuwatendea wanayohitaji. Walipojibu ndiyo, aliwaambia wapokee kadiri ya imani zao. Leo hii wahubiri wanawaita wagonjwa waje wawaombee siyo wawahubiriwe injili. Ndiyo maana wengi hawaponi. Huwezi kupona kwa kuitegemea imani ya mhubiri.Unatakiwa uwe na imani yako. Imani kwako itakuja baada ya kusikia Neno la Mungu. Unataka mafundisho ya injili uijue kweli ikuweke huru. Wacha kuwa na imani tegemezi kwa wahubiri. Imani zetu zinatakiwa kumtegemea Mungu pekee. Ukiiamini Injili, Utubu usamehewe, halafu Mungu akupe uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu, Huwezi kuangushwa kwa madai kwamba unaombewa. Utamuomba Mungu kwa imani yako, na Mungu atakuponya. Soma neno la Mungu kila siku, kwani ndilo litakalokujenga kiimani. Imani yako ikikua, utawaona wengine wakiangushwa na kudanganywa lakini wewe utasimama imara. Yesu alipomfufua Lazaro ilibidi atumie imani yake kwani Lazaro hakuwa hai kuamini. Wewe uko hai. Imani yako inahitajika sana katika kusababisha muujiza wako. Sikiliza sauti yake

Wimbo mpya CCM imewatesa wengi

Wanahabari Wanafiki

MASAI: Hakuna Nuru Gizani!!

Hotuba ya Munishi kwa TAIFA

Washirika Nairobi wa nani?

Nairobi washirika ni sawa na Kondoo waliokosa Mchungaji. Walitoka kwa Mchungaji Mwarandu wakajiunga na Pius Muiru. Sijui waliona nini kwa Muiru, wakahama kwenda kwa James Maina Nganga. Sasa Pastor Nganga anawatingishia funguo za Benzi aliyonunua kwa pesa zao. Nasikia kwamba hata kwa Nganga hawakai. Safari hii sijui wanataka kuhamia kwa nani? Muiru ambaye alikuwa akitamba kuiteka Nairobi na Injili, amejikuta bila wathamini baada ya kundi kubwa la matajiri kulihama kanisa lake. Hata mbinu za kuhubiri imembidi abadilishe. Badala ya mahubiri watu waliomzoea kwayo, sasa Muiru anatabiri kama mganga wa kienyeji. Anakaa mbele ya Camera ofisini kwake, na kuanza kutaja mambo ambayo ni kawaida na ni lazima apatikane mwenye matatizo anayoyatabiri. Mfano akisema kwamba kuna mtu mwanamke mwenye matatizo ya kizazi, na Mungu atamponya kama atatoa shilingi elfu tatu kusaidia huduma ya NURU GIZANI, Lazima watatokea wanawake wengi wenye matatizo kama hayo. Kinachowasumbua wengi akili ni kama baada ya kutoa pesa hizo kweli watapona.

Kundi linalowafadhili wahubiri si watu wengi. Wakiamua kuhama itakuwa vigumu kwa wahubiri kumudu gharama za juu kuendeshea huduma zao.Inasemekana kwamba wahubiri wanaoonekana kwenye TV gharama zao ni Kshs.500,000 kwa juma moja. Sasa matajiri wazito wakihama kama walivyomhama Muiru, Sishangai kumsikia akisema kwenye TV kwamba Bwana amemwonyesha kwamba yule mtu ambaye kanisa limejengwa kwenye shamba lake, asarende hati za kumiliki shamba hilo kwake mara moja, kwani hiyo ni amri kutoka juu kwa Mungu mwenyewe. Wengi walishitushwa na kauli hiyo na wakabaki wakijiuliza nini kitafuatia baada ya kusarenda hati za kumiliki mashamba? Pengine kitakachofuata ni kusarenda wake zetu kwa wahubiri. Mungu asaidie tusifike hapo, lakini kila dalili zinaonyesha tunaelekea hapo. Maisha ya hali ya juu yamewalewesha wahubiri na hawataki kushuka. Lakini Mungu atawashusha.

Wengine wamefikia hatua ya kujitengenezea kile watakachokiita miujiza kwenye TV. Wanachaguliwa watu watakaosema kwamba wamepona ili kuvuta umati kanisani. Wakija wasipone, wanaondoka kimya kimya. Kwa sababu TV bado inatumika kuwatapeli, kila siku hawakosi watu wapya. Wanakamuliwa, wakikauka wataondoka wapishe wengine. Yaani mtindo wa makanisa umegeuzwa na kuwa kama gari la abiria. Linabeba likishusha na hakuna abiria wanaoweza kusema gari ni lao. Makanisa nayo hivyo hivyo yamekuwa ni mali ya wachungaji na familia zao. Washirika hawana lao. Wanachopata ni mafundisho yenye chumvi nyingi, ikiwashinda kumeza, wanaambiwa wameze kwa lazima ya Mungu. Wanatoa na hawaruhusiwi kuuliza pesa hizo zinatumika vipi. Yani Kanisa ni kama KIOSK ya Mchungaji. Anafungua KIOSK asubuhi saa kumi na mbili. Wanaingia kwa maombi ya asubuhi, maarufu kama "Morning Glory" Sadaka asubuhi lazima watoe. Mchana wanakuja maombi ya mchana maarufu kama "Lunch Time Meeting" Hapo pia wataahidiwa ahadi za baraka kutoka kwa Mungu, lakini wao wanapaswa kumbariki Mchungaji wao anunue BENZ ya milioni kumi na tano. Jioni bado watakuja kuombewa baraka pamoja na kupakwa mafuta, kisha wataulizwa kutoa ili kiwanja cha kanisa kinunuliwe. Bei ya kiwanja wataambiwa ni milioni 30 pesa za Kenya. Kila mtu atatoa mpaka akose nauli ya matatu kurudi wanakoishi. Usijali kama kweli kuna kiwanja kinachonunuliwa, au pesa hizo zinatumika kujenga nyumba ya kibinafsi ya mchungaji katika mtaa wa Karen, na hata kama kiwanja kikinunuliwa, na tuna mashaka kama kitanunuliwa, kitakuwa kimesajiliwa kwa jina la mchungaji na siyo Kanisa. Hata washirika wakiamua kumtimua Mchungaji, Hawawezi kulipa madeni ya mamilioni ya shilingi kanisa linayodaiwa na vyombo vya habari ambavyo hurusha vipindi vya mchungaji huyo. Watajiuliza mbona tunachangishwa kila siku kulipia vipindi? Kumbe kwa makusudi Mchungaji halipii vipindi hivyo ili kuwazuia washirika wasije wakawaza kumtimua wachukue usukani Kanisani hapo. Kwa Mchungaji mkimtimua atachukua mkoba wake aondoke awaachie kiwanja ambacho siyo mali yenu, Tena hakuna dalili zozote kuonyesha kwamba kiwanja husika kinatarajiwa kuwa mali ya kanisa, Nadhani wengi watazimia kuambiwa kwamba kiwanja hicho hakijalipiwa chochote. NI ugumu huo ndio unaowafanya washirika wakose nguvu ya kudai haki zao. Nasi tunauliza. Mpaka lini wahubiri matapeli wataruhusiwa kuwaibia watu mchana machoni pa Serikali na kila mtu?

 


Bonyeza hapa usome zaidi

Nyerere Msingi aloujenga Tanzania haufai, Tuubomoe.
Ujamaa ulishindwa, kwani CCM alioanzisha Nyerere sasa imezeeka. Sera zake zimeiharibu nchi yetu Tanzania. Tunataka mapinduzi tuitoe CCM madarakani ili tusinyanyaswe tena. Tumeonewa vya kutosha. sasa basi. CCM hatuitaki, imetufika shingoni. Tutaitapika.Mungu bariki Watanzania, wape hekima ya kutosha kuiweka CCM kapuni. Chukua usukani sasa kuiongoza Tanzania kwani kwa kipindi kirefu nchi yetu iliwekwa wakfu kwa shetani mpinzani wako. Tunamkataa shetani na CCM chama anachotumia kuwatesa watanzania, na tunaiweka nchi yetu mikononi mwako. Tumeomba machache hayo katika jina la Yesu Mwokozi wetu. Amen HABARI ZAIDI



GOSPELGTV.COM
.com

TV ya INJILI
Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM

Tel. 254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com


Hakuna Uchaguzi Tanzania bila Katiba mpya

GOSPELTV WATCH PRO-LIFE VIDEOS


GTV Online

Gospel Television ambayo Studio zake ziko Nairobi Kenya, Sasa itaanza kurusha matangazo yake kutumia Internet. Mipango yote imekamilika na tuko mbioni kukamilisha ile ya kiufundi ili tuwe Online ulimwenguni kote. Endelea kuutupia macho ukurasa huu. Kwa sasa unaweza kuisikia sauti ya GTV. Habari zaidi

Gospel Redio FM
Sasa unaweza kuisikiliza Redio INJILI FM OnLine.
TAHARIRI: Wahubiri Tegemeeni Mungu

Wimbo mpya "Nateseka Natukuza"
"Wanahabari Wanafiki" Wimbo
MASAI: "Hakuna Nuru Gizani" VICHEKESHO
Hotuba ya Munishi kwa TAIFA
"Yesu atakuponya bure" TAHARIRI
Wimbo mpya "Mpende Adui "
GUMZO"Aibu wanahabari!! "


Habari za hapa na pale

Kenedy Ochieng Asema ana UKIMWI Mugabe na Mkapa lao moja
Gospel tape banned by Dar officials Vituko Makanisani Sokoni Gikomba
Munishi Magazetini

Hotuba ya Munishi kwa TAIFA

Ajali ya Kutisha


Moja kati ya ajali mbaya Tanzania HABARI ZAIDI
Gazeti la "MWANANCHI" Tanzania lafichua
www.mwananchi.co.tz

Umewahi kujiuliza kwa nini mabalozi wa Tanzania nchi za nje karibu wote ni wanajeshi wastaafu? Je Serikali huwatumia kufanya ukachero kwenye nchi hizo? Au hujihusisha na mambo ya kidiplomasia kama yalivyo? Je wanajeshi na wanadiplomasia ni taaluma moja? Kwa nini Serikali zote tangu Nyerere zimekuwa zikifuata desturi hiyo? Je ni mbinu ya kuwatawanya wanajeshi ili wasiweke vichwa pamoja kuitoa serikali dhalimu ya CCM? Hayo na mengine mengi, Mwandishi wetu atayaangalia katika makala haya. Habari zaidi

"Standard" Kenya Latoboa siri


Kikwete siyo Wetu!

Wakati Waislamu wameanza kumshuku Kikwete, Wakristo nao wanasema Kikwete siyo wao. Magazeti yenye misimamo mikali ya Kiislamu yamemtaka Jakaya Mrisho Kikwete atangaze msimamo. Ama aachane na Uislamu abatizwe awe Mkristo, au abaki Mwislamu. Walihoji kwamba Kikwete hawezi kuwa na dini zote mbili. Yaani hawezi kuwa Mwislamu Mkristo. Nao Wakristo kwa upande ule mwingine wanashindwa kabisa kumwamini Kikwete kwani wanajua wazi kwamba yeye ni Mwislamu. Habari Zaidi


Zanzibar Kunaashiria Moto

Pastor Pius Kongo Alaumiwa

Pastor Pius Kongo Aliyekuwa TAG Moshi mjini, kabla ya kufungua kanisa lake ambalo sasa wengi wanamtupia lawama. Mwandishi wetu anajiuliza!
Kwa nini wanamlaumu? Je wanaionea wivu huduma yake inayokua haraka? Yuko Mjini Moshi, katika mtaa wa Majengo, nchini Tanzania. Mwandishi wetu alipata nafasi ya kuzungumza na wakazi wa Majengo na kupata maoni yao kuhusu huduma ya Mchungaji Pius Kongo. Pia Kutoka Meru Kenya, Dada Penina ana mengi ya kusimulia baada ya kuhudumu na Mchungaji P.Kongo. Yeye anasema:,
"Safari yangu Moshi yaashiria Moto"


Mwimbaji wa nyimbo za Injili Kutoka Meru Nchini Kenya Penina Muthoni, Akiwa katika ofisi za GTV Nairobi hivi karibuni. Anasimulia masaibu yake alipokuwa Moshi Tanzania akiwa mgeni wa Pastor Pius Kongo. Nao Waciama Vijana mashuhuri wa kuimba nyimbo za Injili Kenya wanasema Walipokuwa Moshi walijionea Mengi.

Sammy Waciama na Jeff Waciama Habari Zaidi


James Kim Atoa kanda mpya

Waislamu wamlalamikia Mwinyi

Aliyekuwa Rais wa awamu ya pili Tanzania Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi Watanzania wanamheshimu kwani yeye ni nyota ya mabadiliko Tanzania. Alikuwa na ujasiri wa kupinga sera za Nyerere akiwa hai, na kuleta mageuzi Tanzania ambayo Mkapa ameyadidimiza matumaini ya Watanzania. Habari Zaidi

"Kikwete Tosha" asema Mchungaji

Mchungaji Paul M.K. Mduma Akiwa katika Ofisi za GTV alielezea masikitiko yake kwamba, vyombo vya habari vimeanza kumchafua Kikwete aliyemjua tangu akiwa mwanafunzi Kibaha Secondary School. Alidai kwamba walisoma wote kwa muda wa miaka minne. Tangu mwaka 1966 hadi 1969 Habari Zaidi

Waruinge Atawazwa Uchungaji

Alikuwa kiongozi wa kundi la Mungiki ambalo Serikali ya Kenya ililiita "kundi haramu" Aliokoka mwaka 2003 na miaka miwili baadaye alitawazwa kuwa Mchungaji Hezekia Ndura Waruinge

Washirika Nairobi wa nani?

Nairobi washirika ni sawa na Kondoo waliokosa Mchungaji. Walitoka kwa Mchungaji Mwarandu wakajiunga na Pius Muiru. Sijui waliona nini kwa Muiru, wakahama kwenda kwa James Maina Nganga. Sasa Pastor Nganga anawatingishia funguo za Benzi aliyonunua kwa pesa zao. Nasikia kwamba hata kwa Nganga hawakai. Safari hii sijui wanataka kuhamia kwa nani? Habari Zaidi

Kikosi cha Living Water Kawe

Waimbaji wa kikundi cha Living Water wakiimba nyimbo za kumtukuza Mungu

Komba Ajikomba na CCM

Wanamwita "Kapteni" Komba Msanii anayetumia sanaa yake kuwatukuza wanadamu badala ya Mungu. Sasa anajuta kuwapandisha wanasiasa ngazi huku mwenyewe akibaki chini.Anasema kama siyo yeye Mkapa asingeuona Urais na hatimaye awe tajiri wa kutisha Tanzania. Mkapa alimsahau Komba mara tu alipoingia Ikulu. Mungu anamwita Komba amtumikie. Uzee unapomnyemelea Komba, laiti angeona mwanga amtukuze Mungu badala ya wanasiasa waongo.Kila la Kheri Bwana Komba.

Padre Atuhumiwa kwa UBASHA

Padre Sixtus Kimaro Akiwa mahakamani Kisutu Dar.
Ameshitakiwa kwa tuhuma za kumlawiti mvulana wa miaka 17
Sisi tunasema "Lisemwalo Haliko, Kama liko, Lilikuwepo." HABARI ZAIDI

Simbeye Mchawi Aliyeokoka


Bwana Zebius Mulingwa Simbeye Akiwa na Joyce Wairimu Maina Kericho Kenya


Mtoto apatapo Mtoto


Siri za Kakobe



Askofu Nnko ailalamikia Serikali


Kuishi Amerika ni haki yako


Samples. 6 second of every song

SIDE A

  1. Mpende Adui
  2. Wahariri Watubu
  3. Yesu Bima Tosha
  4. Kuhubiri ni Taluma
  5. Maji Yana Mdudu
  6. Gazeti Siyo Ugali

SIDE B

  1. Yesu Aponya
  2. Jirani Mchokozi
  3. manabi.wav
  4. Rushwa Adui
  5. Msiabudu Amerika
  6. Baba Nakuabudu

SIDE A

  1. Malebo
  2. Usichanganye
  3. Yesu Mambo Yote
  4. Ukimwi Na Maisha
  5. ? Wanamwabudu Nani ?

SIDE B

  1. Yesu Nakupenda
  2. Mageuzi Na Injili
  3. Kazi Na Wanawake
  4. Maombi
  5. Yesu Mwanzo Na Mwisho

SIDE A

  1. Yesu Aliniita
  2. Bwana Nashangaa
  3. Tuonane Milele
  4. Wamwendea Yesu
  5. Msalabani Pa Mwokozi
  6. Yesu Kwetu Ni Rafiki

SIDE B

  1. Bwana Uliyewaita
  2. Kumtegemea Mwokozi
  3. Sioni Haya Kwa Bwana
  4. Yesu Unipendae
  5. Yesu Nakupenda
  6. Ati Tuonane Mtoni

SIDE A

  1. Makosa Ni Kosa
  2. Fikiri Mwanadamu
  3. Dhambi Ni Nini
  4. Yesu Anaokoa

SIDE B

  1. Ajirekebishe
  2. Kaka Ananitesa
  3. Christmas
  4. Anarudi Yesu

SIDE A

  1. Chini Ya Mwamba
  2. Paulo Na Sila
  3. Kifo Mapatano
  4. Nimekukimbilia Nisiaibike
  5. Upendo Ule Wa Kwanza

SIDE B

  1. Salama Rohoni
  2. Hakuna Mungu Kama Wewe
  3. Nimuogope Nani
  4. Huna Cha Kujivunia
  5. Amua Mwenyewe

SIDE A

  1. Ninyime Vyote Niachie Yesu
  2. Maisha Yalitisha
  3. Fashoni Ni Yesu
  4. Anakuita
  5. Waokoe Vijana
  6. Uliyaona Zamani?

SIDE B

  1. Ulimi
  2. Pesa
  3. Dhambi
  4. Siku Za Mwisho
  5. Nielezeje

Gospel Television Moto wa kuotea mbali

Ikiwa ndio kwanza inajitayarisha kurusha matangazo yake, GTV imekuwa tishio kwa Serikali Tanzania. Aliyekuwa Rais wa kimabavu nchini humo William Benjamin Mkapa aliamuru polisi wawatie mbaroni wote watakaopatikana na VCD za GTV. Kisa ni kwamba Gospel Television ilikuwa imezungumzia uwezekano wa Mkapa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kutumia madaraka vibaya. GTV ilikuwa imedai kwamba, Mkapa akiwa madarakani aliwaamuru POLISI wawaue Wazanzibari zaidi ya 70 kwa kosa la kusema CCM Chama Cha Majambazi hawakitaki. Pamoja na mambo mengine GTV ilipendekeza tume ya kumchunguza Mkapa iundwe na akipatikana na makosa sheria ichukue mkondo wake. Pia GTV ilidai kwamba Mkapa aliitawala Tanzania kama mali yake binafsi kwani hakutaka ushauri wa mtu yeyote. Bado msimamo wa GTV ni huo na hatuombi msamaha kwa Mkapa wala CCM. Habari Zaidi
Hotuba ya Munishi kwa TAIFA

Twende nikutembeze Nairobi

 

 
| http://munishi.com |