Ukurasa wa mbele
Soma barua Yahoo
Soma barua Hotmail

 



GOSPELGTV.COM


TV ya INJILI
Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM

Tel. 254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com

Kimurgor Ameuawa

Aliyekuwa Mlinzi mkuu wa Moi Bwana Kimurgor, ameuawa mjini Nairobi. Commando aliyesomea Israel, pia aliwahi kuwa mkuu wa kikosi cha GSU wakati wa utawala wa Rais mstaafu Moi. Wakati serikali ya Kibaki ilipochukua madaraka, Bwana Kimurgor alistaafishwa na kuwa raia wa kawaida. Mpaka siku ya kufa kwake, alikuwa ofisa ulinzi katika kampuni binafsi ya ndege. Inasemekana kwamba alikuwa akiendesha mwenyewe ndani ya gari yake aina ya TOYOTA PRADO katika mtaa wa Fedha Estate, alipokutana na watu watatu wenye silaha.Aliposimamishwa na watu hao, alihisi hatari na kukaidi amri yao. Aliendesha kasi kuwapita lakini commando safari hii hakuwa na bahati kwani walimfyatulia risasi zilizoyakatiza maisha yake papo hapo.Polisi wameanza msako mkali, huku vyombo vya habari vikiripoti kwamba wauaji wake walikuwa majambazi wa kawaida. Ila hakuna chochote kilichoibiwa kutoka kwa marehemu. Hata silaha yake aina ya pisto ilikutwa ikiwa sawa na risasi kumi na moja ndani yake, jambo linaloonyesha kwamba commando hakuweza kuitumia silaha yake kujikinga na watu waliopania kumuua.

Nchi za Kiafrika marais hulindwa na watu kutoka Kabila lao kama siyo ndugu zao wa kuzaliwa.Hata kama hawana taaluma hiyo ya ulinzi, Pesa za Serikali hutumika kuhakikisha wamepata mafunzo husika. Rais akiachia madaraka basi walinzi wote wa rais hufutwa kazi kama siyo kuuawa. Ikiwa madaraka yalichukuliwa kwa nguvu, basi walinzi wote wa rais hukimbilia uhamishoni kwani wanakijua kinachowangoja. Hiyo ndiyo Afrika yetu. Badala ya kuwafundisha wazalendo wanataaluma ya ulinzi bila kujali kabila lao, usishangae hata mkuu wa majeshi katika nchi nyingi za Kiafrika lazima atoke kabila la Rais au awe ndugu wa karibu.Nani aliwadanganya Waafrika kwamba ndugu wa karibu hawezi kuwageuka? Tena nani aliwapotosha kwamba watakuwa salama mikononi mwa watu wa kabila lao? Siyo ajabu viongozi wengi Afrika hawataki kutoka ikulu wakishaingia.Wanahitaji miaka mingi kuweza kuwaandaa ndugu zao waweze kushika nyadhifa zote muhimu katika nchi.Wakitoka madarakani, Yule atakaeingia haijalishi amesoma kiwango gani, Bado atafuata utamaduni huo huo wa kijinga. Kubadili wakuu wote wa vikosi vya ulinzi, Hata jaji mkuu lazima atoke karibu na kijijini kwao. Usiwahi kutegemea haki katika vyombo vya sheria Afrika. Inategemea unamjua nani. Nasikia hata nchi zilizoendelea mambo hayatofautiani sana na Afrika. Badala ya Ukabila, wao wanatumia matabaka na kwingine ubaguzi wa rangi Wakati mwingine dunia inaweza kuwa chungu sana hasa ukiwa na mawazo huru yasiyoegemea upande wowote.

Wanahabari nao hawakuachwa nyuma katika uoza huu. Serikali nyingi Afrika huakikisha zina ajenti wao katika kila chombo cha habari nchini .Ndiyo maana vitendawili haviishi kila kukicha. Utasikia "fulani ameuawa na majambazi wa kawaida, baada ya kuwakuta wameshampora gari mama mwingine, na walipotaka kutoroka wakitumia gari ya marehemu; inaonekana marehemu alikaidi amri ya majambazi hao wa kawaida; na ndipo walipomfyatulia risasi na kumuua, bila kuchukua chochote. Hata Bunduki ya marehemu haikuchukuliwa. Tunawaomba wanainchi muwe watulivu kwani serikali haihusiki kabisa na mauaji hayo ila ni majambazi wa kawaida."

Swali ambalo mtu anaweza kujiuliza ni, Ilikuwaje vyombo vya habari vikawa vinawajua majambazi wa kawaida na wale wasio wa kawaida? Je nchi inapaswa kuwa na hao majambazi wanaoitwa wa kawaida? Mbona wanatuarifu kana kwamba wanataka ushahidi fulani uonekane? Yaani wamekazania majambazi wa kawaida, kana kwamba serikali haiwezi kutayarisha mauaji yaonekane watakavyo. Katika nchi za Kiafrika tumeona mengi.Tumewaona viongozi waliouawa na kisingizio kikawa ni ajali za barabarani. Wengine walipewa sumu na kisingizio kikawa ni shinikizo la moyo. Wengine walipelekwa ngambo na walipouawa huko, kisingizio kikawa ni maghaidi na wauza madawa ya kulevya waliommaliza baada ya kuwatapeli.

Mambo ni mengi. Na wanasiasa husema njia za kuua panya ni nyingi. Tunaomba isiwe kwamba Kimurgor naye amemalizwa kwa moja ya njia hizo.


"CCM Wakiniua Mnizike Kenya"
"CCM Wakiniua, Mnizike Kenya." Asema Munishi. "Siyo kwamba nimebadili uraia, wala sitarajii kufanya hivyo.Mimi bado ni Mtanzania. Sikuchagua kuzaliwa Tanzania, lakini nitachagua pa kuzikwa.Serikali za CCM zimenifanya nisiwe na mahali ninapoweza kupaita nyumbani ndani ya nchi yangu. Kosa langu ni kusema CCM sera zake zimeiharibu Tanzania, na hawafai kuwa madarakani.Makachero wa Tanzania wamekuwa wakitumia kila mbinu chafu kuwasumbua na hata kuwaua wote walio na uhusiano wa karibu na Munishi. Ajabu ni kwamba Munishi mwenyewe akienda Tanzania wanafuatilia nyendo zake bila kutishia kumuua. Akiwa Kenya ambako ndipo sanaa yake ilimpatia uwezo wa kununua nusu ekari ambapo amejenga nyumba ya mabati kujisitiri na jamii yake, bado makachero hawaishi kumvamia kama majambazi, na kutishia kumuua. Munishi akiwaeleza wanahabari kwamba wavamizi walidai kutumwa, wao wanaandika kwamba ni majambazi wa kawaida. Walijuaje kama ni majambazi wa kawaida? Tena wangejuaje kwamba siyo majambazi wa kawaida? Basi kwa nini waandike ni majambazi wa kawaida? Mbaya zaidi wanasema Munishi ndiye aliyewaambia wakati sivyo. Mtu akikuuliza je! unaona waliokuvamia kama ni washindani wako kibiashara? Na jibu likawa ni vigumu kujua kwa hakika wavamizi wangu ni kina nani, Lakini walidai kutumwa na watu ambao hawakuwataja. Je hapo utakuwa umesema kwamba majambazi hawakuwa washindani wangu kibiashara bali ni wa kawaida? NATION wanapaswa mara moja kumjibu Munishi kwani mahojiano aliyanakili kwenye simu yake

 

 
| http://munishi.com |
 
ss