Please Wait

GOSPELGTV.COM

Gospel TV BANNED IN TANZANIA
WORLD NEWS


Visit My Message Board

Contact us/
Tuandikie

Rev.Mtikila na Urais Tanzania


Kakobe Anayahonga Magazeti?

Askofu Kulola kada wa CCM?


Bishop Deya MATATANI

Mjue Bishop Arthur Kitonga


Pastor Nduati John Kigoi Afikishwa mahakamani kwa utapeli


Pastor Mwangi Aiaga Dunia Ajalini

Salim Rais mtarajiwa?

Serikali Kenya yatishia kubomoa kanisa la Pastor Muiru Yeye Husema KUNA NURU GIZANI Lakini sasa inaonekana giza nuruni

HABARI NYINGINE MOTO MOTO

CNN
TBN
BBC
Times
Islamtz.org
Winners
Maranatha
Intergrity

China Today

Japan Times

Korea Online

China Site

China Maps

USA Today

China English

Gv China

China view

China news

China
Natinal
News

China Tech

India News

India Times

India Daily

Gospel of
Jesus

USA Gospel

Gospel
Church

Dubai news

Africa News

Gospel Music

US VISSA

BBC
Bush
Curches
Gospeltv
munishi
Mkapa
usgospel
Times
GTV
GTVGOSPEL
Jesus
God
Faith
Life
Kenya
Tanzania
Uganda
Africa
Japan
Toyota
China
Korea
India
Nation
News
Online
Nyerere
Kibaki
Museveni
Mugabe
KOFFI ANNAN
Nairobi
Dar
Goverments

gospel TV

gospelradio

Gospel radio

gospelnews

Gospel news


Jesus Loves You Welcome to GOSPELGTV.COM


.com


TV ya INJILI
Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM

Tel. 254722602445 E-mail:
munishigtv@gmail.com or munishi@gospelgtv.com


Matukio FaceBook


TVT NI TV YA TAIFA AU YA CCM?


Wanahabari Tanzania, hasa wale wanaofanya kazi katika vyombo habari vya serikali, ni vibaraka wa serikali. Wanaegemea upande wa serikali hata kama serikali husika inakiuka haki za binadamu. Tangu enzi za Nyerere vyombo vya habari Tanzania viligeuzwa kuwa wasemaji wa serikali. Nyerere aliitumia sana redio Tanzania Dar es Salaam kueneza injili yake ya ujamaa na kujitegemea. Matokeo yake yakawa ni kushindwa vibaya kwa siasa ya ujamaa jambo lililopelekea afya ya Nyerere kuzorota na hatimaye kuiaga dunia. Soma Zaidi




Mbunge wa CCM (viti maalum) Bi Amina Chifupa akanusha kwamba amemuacha mumewe Bwana Mohamed Mpakanjia, na kuwa kimada wa Rais Kikwete. Alisema wanaoeneza uvumi huo wana nia ya kumwaribia ndoa yake. Hii ni kufuatia taarifa ya vyombo vya habari kwamba mbunge huyo sasa ana nguvu kuliko Rais mwenyewe. Cha ajabu ameanza kuwapa tumbo joto hata wabunge wenzake kutoka chama tawala. Usijali kwamba hakuchaguliwa na wananchi, Lakini aliyemteua bungeni alijua kwa nini alifanya hivyo. Pengine ni kwa sababu ya dini yake, au urembo wake, na kuna wale wanaoenda zaidi na kusema ni kwa sababu ya misimamo yake katika masuala ya kijamii.Vyovyote vile, lakini sisi tunasema adui wa adui yako ni rafiki.Soma Zaidi

Bishop Ndzomba afungua makazi ya watoto yatima
SUSTAINABLE SOLUTION FOR THE KENYAN ORPHANS.


Bishop Robert Mdzomba afungua kituo cha watoto yatima Kenya. Asema ni uvumbuzi wa kudumu kwa wale wasiobahatika katika jamii. Atoa mwito kwa wahisani wauchangie mradi huo kwa moyo wa kuwajali wengine. HABARI ZAIDI

Kiboro ametoka Nation yakarabatiwa


Gazeti la Nation kwa mara nyingine wamegeuza sura, Baada ya mkurugenzi wa zamani bwana Wilfred Kiboro kunyeshwa mlango. Mkurugenzi mpya amekuja na mbinu mpya. Ana kibarua kizito kurudisha heshima ya Nation kama gazeti linalozingatia maadili ya taaluma ya uandishi habari Soma Zaidi



"CCM Wakiniua Mnizike Kenya"Asema Munishi

Msafara wa Moi ajalini


Rais Mstaafu wa Kenya Mheshimiwa Daniel Toroitich Moi, akiuguza majeraha aliyoyapata kwenye ajali iliyohusisha msafara wake, lakini gari iliyogongwa ni ile iliyokuwa imembeba yeye.Maswali mengi yameulizwa, lakini majibu yake yatatoka kwa mkuu wa Polisi. Iweje gari iliyombeba RAIS igongwe wakati zile za walinzi ndizo zilizopaswa kugongwa zikimlinda RAIS? Je lilikuwa jaribio la kuyakatiza maisha ya Moi? Kibaki Rais wa sasa Kenya analionaje hilo? Marekebisho gani serikali itayafanya katika kikosi kinachomlinda Rais wa zamani? Kuna mtu atakayefutwa kazi kufuatia ajali hiyo? Habari zaidi

Kibaki achaguliwe tena?
Machozi ya Uhuru


Kiongozi wa Upinzani Kenya Bwana Uhuru Kenyata akilia machozi ya Uhuru
Tatizo la wachuuzi halitafutiwi dawa makusudi. Wanasiasa huwatumia wachuuzi wakati wa uchaguzi.Wengi wa wapiga kura katika nchi za Afrika ni masikini wanaojitafutia riziki kwa njia za kuchuuza biashara ndogondogo. Siyo dhambi kufanya hivyo. Wafanyibiashara wakubwa huanza kwa kuchuuza kwanza. Kwamba wanasiasa watawaamuru polisi wawamiminie wachuuzi risasi za moto vichwani, hilo linatisha. Sambamba na hilo, hatuungi mkono hatua ya wachuuzi kulipiza kisasi kwa kumuua askari polisi. Wote wamekuwa wauaji. Lakini haiingii akilini kuona polisi wa kenya wakiwaua raia wa Kenya kwa kosa la kujitafutia riziki zao za kila siku. Hata kama Nairobi inatakiwa kuwa safi, lazima usafi huo uwe wa kiwango cha nchi changa za kiafrika ambazo umasikini uko kwa kiwango cha kutisha. Kuigiza usafi wa miji ya nchi zilizoendelea, kutaigawa nchi katika matabaka ya matajiri wachache wasiotaka kuona masikini karibu nao. Tunaomba isifikie mahali pa kutungwa sheria inayosema kuwa masikini ni kosa linalopaswa kuadhibiwa kwa kupigwa risasi kichwani au kifuani? Habari Zaidi

Gharama ya kuwa na gari Nairobi

Siku hizi ukifanya kosa barabarani, utakutana na hawa jamaa. Watakupiga, halafu wataamua wakushitaki kwa kosa gani, na kisha upelekwe mahakamani kama hutaongea lugha wanayoijua.
Kabla uamue kununua gari Nairobi, Siyo vibaya ukajifahamisha unatakiwa kuilipia kiasi gani kwa siku. Kwanza kupata mahali pa kuliegesha lazima umlipe atakayekuonyesha mahali hapo KSHS 30 na kuendelea. Kisha askari wa tume ya jiji naye utamlipa KSHS 70 kila siku na ninasikia gharama hiyo itaongezeka kufikia KSHS 200 kwa siku. Ukifikiri umemaliza kulipa, bado unatakiwa ulipe KSHS 50 na kuendelea kwa mlinzi atakayekulindia taa za gari lako pamoja na vibandiko vinavyoonyesha gari yako ni aina gani zisingolewe. Ukipuuzia, yeye huyo huyo ndiye atakayefanya mpango gari yako iwe haina vibandiko kwenye magurudumu, au taa za kuonyeshea ishara utazikuta hazipo. Ukifikiri yataishia hapo, kuna yule atakaekuombea nafasi kwa wenye magari wakupe nafasi ya kutoka ulipoliegesha gari lako. Huyo hupokea chochote. Sasa unaweza kuelekea nyumbani, na ni kama hukufanya kosa lolote la trafiki ukamatwe. Kama utakuwa umekamatwa basi kiwango unachotakiwa kubeba kwa siku siyo chini ya KSHS 20,000 ili uwe salama pande zote. Ukikosa kiwango hicho, usishangae siku moja utakosa kurudi nyumbani, na watakapokutafuta hospitalini wakukose, tena wakutafute chumba cha maiti wakukose, basi wakienda jela watakukuta umefungwa miezi miwili au mitatu kwa kosa la wewe kuwa na gari bila kubeba KSHS 20,000 kila siku kukufanya uwe salama. Na hapo ni kama hujagonga Benzi ya mtu nyuma uvunje taa moja tu ya nyuma. Kama gari yako ni kama yangu, basi itauzwa, na bado haitatosha kuilipa taa moja ya Benz. Pole nimesahau mafuta ya petroli na Oil na mafundi kama itaamua kukataa kunguruma kwa sababu zozote. ZAIDI


Kikwete Ameanza wizi
Anaendeleza mbinu za Nyerere kuwatisha raia


Miezi mitatu madarakani, Kikwete ameanza kutumia mbinu za Nyerere kuwatisha raia Tanzania. Anawatuhumu wananchi kwamba mali walizo nazo hawakuzipata kihalali. Hii ni mbinu ya Serikali kuhakikisha mali zote Tanzania ziko mikononi mwa watu wanaodhaniwa siyo tishio kwa CCM. Ni zoezi la kisiasa kukiimarisha chama tawala. Kwamba Kikwete anatumia mbinu hizo wakati huu, inashangaza. Nchini Tanzania wenye mali kihalali ni wanachama wa CCM na viongozi wake. Wengine wote hata kama siyo wanachama wa chama chochote cha kisiasa, wakiwa na mali CCM hawalali usingizi. Watatunga mbinu za kuwaita majambazi wakati wenyewe ni majambazi nambari wani.

Kibaki ajenga Hospitali ya kisasa Nairobi


Dr. Dan Gikonyo na mkewe Betty, mbele ya hospitali ya kisasa iliyojengwa katika mtaa wa Karen Nairobi. Dr. Gikonyo ni daktari binafsi wa Rais wa Kenya Mheshimiwa Mwai Kibaki. Hospitali hiyo yenye mitambo ya kisasa, inasadikiwa kuwa ya kipekee Afrika. Inaweza kufanya mambo mengi ambayo viongozi wa Afrika hulazimika kwenda ngambo kutibiwa. Kwamba Kibaki alifikiria kujenga hospitali kama hiyo Kenya, ni hatua inayostahili kupongezwa. Lakini gharama za matibabu katika hospitali hiyo ni za juu kiasi kwamba matajiri tu ndio watakaoweza kumudu. Itambidi Kibaki afikirie jinsi ya kuiboresha hospitali ya Kenyatta ambayo ndiyo hospitali ya rufaa nchini Kenya ili wananchi wa kawaida waweze kumudu gharama za matibabu. Vinginevyo itaonekana kwamba matajiri pekee ndio wanaostahili kuishi Kenya, na wengine wapotelee mbali. Zaidi


Nyumba yaporomoka Nairobi


Back to School But...

Anaitwa Ruth Wanjiru. Anamlilia mama asimwache Shuleni. Mpiga picha BONIFACE MWANGI alipokuwa katika ziara ya shule za Nairobi, alimkuta Ruth akijigaragaza chini akilia.Kwake, ni nani kama mama? Japo jina la Shule ni GLAD TOTO NURSERY SCHOOL, ikimaanisha toto lenye furaha, Wanjiru alionekana kutokuwa na furaha siku yake ya kwanza Shuleni hapo. Sababu ni kwamba kuna watu walioamua kumtoa nyumbani na kumpeleka shuleni bila matakwa yake. Haijalishi wazazi wanapenda kiasi gani watoto wao waende shule, Lakini kama watoto wenyewe hawajui maana ya shule, watakuwepo kuwaridhisha wazazi, na elimu ya kweli wataipata watakapohitaji au watakapolazimishwa na hali ya maisha. Je tuwaache watoto mpaka watakapoiona maana ya elimu ndipo tuwapeleke Shule?
Habari Zaidi


Kikwete Azimia
Azimia Jangwani kwenye mkutano wa lala salama, Magazeti yaandika ana UKIMWI, Wengine wasema Mwisho umeifikia CCM. Wengine wasema ni Mkono wa Mungu kuwafundisha adabu CCM

Walikuwa wakimsikiliza Kikwete kwa makini. Uwanja ni Jangwani jijini Dar. Ilikuwa siku moja kabla ya uchaguzi. Akiwa katikati ya hotuba yake iliyokuwa ikirushwa moja kwa moja kwenye TV na Redio Tanzania, Kikwete aliomba maji. Kabla ayafikishe mdomoni, magoti yalililegea na kuuacha mwili wa Kikwete kupigiza chini kama nyani aliyekosea tawi. Mkapa na walinzi wa kikwete walipigwa na butwaa kiasi cha kubaki midomo wazi. Umati ulionekana kuchanganyikiwa wasijue cha kufanya. Walinzi walikurupuka kumkimbilia Kikwete ambaye tayari alikuwa chini. Waliwaamuru wapiga picha waelekeze kamera zao kwa wananchi wakihofia kwamba Rais mtarajiwa ameiaga dunia. ITV kibaraka wa CCM walikatiza matangazo yao. TVT TV ya Propaganda za CCM nayo haikuwa na jinsi ila kuwatangazia watazamaji kwamba Kikwete alikuwa mzima na wasiwe na wasi wasi. Bila kujua kwamba matamshi hayo ndiyo yaliyowapa watanzania wasiwasi. Hata Kikwete alipoongea masaa mawili baadaye, watu hawakuamini ni yeye. Ndiyo maana wana CCM wengi hawakujitokeza kupiga kura wakihofu watakuwa wakichagua kivuli na siyo Kikwete. Kwa sasa mtizamo wa Watanzania ni kwenye AFYA ya Kikwete. Je ni mgonjwa kama ilivyodhaniwa? Habari Zaidi



KIBAKI AJICHIMBIA KABURI KISIASA
Kosa la Simba kumwachia fisi windo lake
WAKENYA WASEMA NO KWA KATIBA KIELELEZO- PIGO KWA KIBAKI

Wahenga zamani walisema, Simba ni mwindaji hodari.Akifanya kosa la kumwachia fisi windo lake, Basi mafisi wataitana kwa kicheko, na kabla simba ajue nini kinaendelea, wingi wa fisi utamzuia kujaribu kudai windo lake. Pengine arudi msituni akawinde, au afe njaa. Kusema ajaribu kunyakua windo mdomoni mwa fisi, atahatarisha maisha yake. Isitoshe mabaki aliyoacha fisi, hayafai kuliwa na yeyote.Mfupa uliomshinda FISI hata simba hauwezi. Bora akawinde. Inaonekana Raila ameamua kuwinda na tayari amepata. Kama kawaida KUNGURU Fisi na Mbwa mwitu wanajiandaa kujaribu bahati yao ili wapewe ngaa mnofu kidogo.Swali ambalo wengi wanajiuliza ni je safari hii atakubali kuachia windo lake kwa yeyote? Tunasubiri tuone.Habari zaidi

Mchungaji Alaani Mauaji Zanzibar

Mchungaji Mmasi wa TAG Kibosho Moshi nchini Tanzania, Amelaani vikali mauaji ya kisiasa yaliyofanyika Zanzibar hivi karibuni. Akiongea na GOSPELGTV mjini Nairobi, Mchungaji Mmasi alisema kwamba serikali ina mkono mrefu, lakini mkono huo unapotumika kuwanyamazisha wapinzani kwa gharama yeyote, hapo ndipo serikali inapokosea. Aliitaka Serikali ya CCM ijue kwamba mkono wa Mungu ni mrefu kuliko wa serikali. Habari Zaidi


CCM Wameanza kuua tena
Nchini Tanzania Wanaopinga CCM chama kinachotawala kwa mabavu, Wanauawa.


Chuki ambayo Serikali ya CCM inaipanda mioyoni mwa Watanzania, siku moja watavuna matunda yake. Mkapa anamaliza muda wake vibaya. Asifikiri wale anaowatesa akiwa madarakani, watamwacha aishi salama wakati atakapoachia madaraka. Pesa alizowaibia Watanzania zitakuwa chungu kila senti. Inashangaza Amerika wanamsakama Saddam Hussein na wanamwacha Mkapa awaue Watanzania apendavyo. Mungu atatulipizia kisasi.

Chuo Kikuu wasema 'NO' kwa CCM

(Picha na Mroki Mroki)
Wanachuo wa Chuo Kikuu Dar es Salaam UDSM wakiandamana Dar kupinga sera za Serikali ya CCM.Wanaitaka Serikali kupitia bodi ya udhamini wa wanafunzi wa elimu ya juu HESBL, Kuwalipa haraka pesa zao za kujikimu.Walidai hiyo ni haki yao na hawaoni sababu ya Serikali kutumia pesa za walipa kodi kufanyia kampeni za CCM, huku wanafunzi na wananchi wakishindwa kujikimu kimaisha.Walisema Tanzania siyo mali ya CCM na TRA, bali ni ya Watanzania wote na wanachuo wakiwemo. Waliongeza kwamba hawaoni sababu ya kuirudisha CCM madarakani ikiwa mbinu zao ni kuitumia TRA kama silaha ya kuwatisha wananchi ili iwaibie mali zao. Walisema kwamba wanafunzi na wananchi wamekondeana kwa njaa, huku viongozi wa CCM na wafanyikazi wa TRA wakivimbisha matumbo kwa pesa za umma. Walionya kwamba wizi huu wa mchana lazima ukome. Habari Zaidi

Meet The Kioko's

Bwana anapofanya kazi tofauti na mkewe, lakini bado wanakuwa na lengo moja. Habari Zaidi

Hakuna Uchaguzi Tanzania bila Katiba mpya

Mchungaji Faustin Munishi amesema hakuna Uchaguzi Tanzania bila Katiba mpya. Akiongea katika Gospel GTV Pastor Munishi alivitaka vyama vya upinzani Tanzania kuususia uchaguzi kwani CCM wakitumia katiba ya sasa wameumaliza upinzani Tanzania. Kwa sasa ni sawa na hakuna upinzani. Kuingia kwenye uchaguzi ambao CCM hawaruhusu wengine waseme, ni sawa na kuwafunga vifaranga wa kuku na kuwashindanisha na mwewe. Matokeo mnayajua. CCM wanajua walichofanya Tanzania kwa miaka zaidi ya arobaini, ndiyo maana wananunua kila mtu. Pesa zilizo haki ya mikoa kimaendeleo, zinatumika kuinunua mikoa iiunge mkono CCM. Alisema lazima Katiba ibadilishwe kuwaruhusu wagombea binafsi ndipo upinzani wa kweli utakapoonekana Tanzania. Alielezea nia yake ya kugombea Urais Tanzania bila chama cha kisiasa. Mchungaji Munishi alisisitiza kwamba "Siasa ni uongo na hawezi kujiunga na uongo ili awatoe waongo." Alisema kwamba endapo CCM watakaidi kuibadili Katiba, basi wafuasi wake watamtangaza rasmi kuwa Rais wa Gospel Tanzania. Kwa mara ya kwanza Tanzania itakuwa na marais zaidi ya kumi. Huko ndiko tunakoelekea ikiwa CCM watawaburuza watanzania kwenye uchaguzi bila KATIBA mpya. Habari Zaidi

Munishi awasili Tanzania

Mwinjilisti na mwimbaji wa Nyimbo za injili Faustin Munishi yuko nchini Tanzania. Aliwasili Mjini Arusha tarehe 4/10/05 kwenye basi la kampuni ya Scandinavia.Anatazamiwa kutua Dar es salaam ambako atatangaza msimamo wake kuhusu uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanywa mwezi huu. Awali Mchungaji Munishi aliwahi kuviambia vyombo vya habari kwamba yeye anapinga uchaguzi Tanzania bila katiba mpya.Alisema kwamba katiba ya sasa ina ujanja mwingi wa kuirudisha madarakani CCM kiulaini. Alielezea masikitiko yake kwamba upinzani Tanzania umemalizwa nguvu kwa hila za CCM wakiitumia katiba ambayo Nyerere aliigeuza ilinde maslahi ya CCM hata kama yeye ni marehemu.Kwamba msimamo wake bado ni huo, hiyo itajulikana atakapowasili Dar.

CCM sasa ni 'Mzoga'

Yalianzia viwanja vya KARIMJEE Dar es Salaam, na kumalizikia Mnazi Mmoja. Yalikumba wa kila rika.Walisema ni maandamano ya kuchangia watoto yatima, Lakini ujumbe kutoka mioyoni mwao ni kwamba CCM OUT.Watanzania wengi wamechoshwa na KERO za CCM. Woga unawafanya waseme wasiyomaanisha.Siku ya kufa nyani, miti yote huteleza. CCM ni Nyani ambaye siku ya kufa kwake imefika. Haijalishi ujuzi wa miaka arobaini kuparamia miti, Lakini safari hii miti yote inateleza. Watapigiza chini kwa kishindo, na ndio mwisho wao. Watanzania tunataka ENZI MPYA bila CCM. Habari Zaidi

Kimurgor Ameuawa

Aliyekuwa Mlinzi mkuu wa Moi Bwana Kimurgor, ameuawa mjini Nairobi. Commando aliyesomea Israel, pia aliwahi kuwa mkuu wa kikosi cha GSU wakati wa utawala wa Rais mstaafu Moi. Wakati serikali ya Kibaki ilipochukua madaraka, Bwana Kimurgor alistaafishwa na kuwa raia wa kawaida. Mpaka siku ya kufa kwake, alikuwa ofisa ulinzi katika kampuni binafsi ya ndege. Inasemekana kwamba alikuwa akiendesha mwenyewe ndani ya gari yake aina ya TOYOTA PRADO katika mtaa wa Fedha Estate, alipokutana na watu watatu wenye silaha.Aliposimamishwa na watu hao, alihisi hatari na kukaidi amri yao. Aliendesha kasi kuwapita lakini commando safari hii hakuwa na bahati kwani walimfyatulia risasi zilizoyakatiza maisha yake papo hapo.Polisi wameanza msako mkali, huku vyombo vya habari vikiripoti kwamba wauaji wake walikuwa majambazi wa kawaida. Ila hakuna chochote kilichoibiwa kutoka kwa marehemu. Hata silaha yake aina ya pisto ilikutwa ikiwa sawa na risasi kumi na moja ndani yake, jambo linaloonyesha kwamba commando hakuweza kuitumia silaha yake kujikinga na watu waliopania kumuua. Habari Zaidi

Mkurugenzi wa EATV afariki
Je alitolewa sadaka kwa Shetani?
Web Site ya Gospel kusheherekea machungu ya wengine?


Mkurugenzi mtendaji wa East africa TV na Redio bwana Rodney Mutie Mengi amefariki mjini Dar es salaam Oktober 6 2005. Bwana Mengi mwenye umri wa miaka 31, atakumbukwa na wapenzi wa muziki katika EATV. Akiwa mkurugenzi, EATV pamoja na redio yake ilishika kasi katika miji mikuu ya mataifa ya Afrika ya Mashariki. TV hiyo ambayo imekuwa maarufu kwa kuonyesha miziki ya kidunia inayotukuza ngono na ufahari, ilikuwa kero kwa waumini wa dini. Haikujulikana mara moja kilichosababisha kifo chake, ila Taarifa tuliyoipata kutoka gazeti la NIPASHE, ilimkariri baba wa Marehemu ambaye pia ni mmiliki wa utitiri wa vyombo vya habari akisema kwamba mwanawe ameiaga dunia. Tangu kifo chake, Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Mengi baba wa Marehemu, vimekuwa vikiripoti watu mashuhuri waliofika kutoa rambirambi zao badala ya kuelezea kilichosababisha kifo cha Mkurugenzi huyo. Tayari kuna uvumi mitaani, lakini GOSPELGTV inawaomba wanaoeneza uvumi waache. Wakati huu wa majonzi utumike kuwapa pole jamaa na marafiki wa marehemu, ili kama EATV itampata mkurugenzi mpya, asikie kilio cha wengi kwamba TV hiyo inaupotosha umma kwa miziki yao inayotukuza picha za ngono. Ikiwezekana wazipatie nyimbo za GOSPEL kipau mbele na Mungu atawabariki. Hata hivyo GOSPELGTV tunawapa pole jamaa na marafiki wa marehemu. Mungu anajua pa kuiweka Roho ya Marehemu. Maombi yetu hayatabadilisha hilo.Habari Zaidi

Rufftone wapambana na Ringtone
Walipotangaza vita magazeti yote yaliandika. Sasa wanadai kupatana, magazeti yote kimyaaaa!!

Rufftone wakiwa na Ringtone Kisii

Roy Smith Mwatia na Alex Apoko
Ni MARAPA wa Gospel. Usijali majina yao ya Kiluhia na Kikamba, Lakini wanajulikana kama Rafftone na Ringtone.Kila mmoja anadai kumzidi mwenzake katika kurap Gospel.Wanachosahau ni kwamba wote ni mapandikizi ya vyombo vya habari. Siku Media itawaweka chini, Huo utakuwa mwanzo wa mwisho wao.Pengine wajikaze kiusanii wakite mizizi yao wenyewe. Lakini kwa mtindo huu wa kujiona wamefika, tena mbaya zaidi wanajilinganisha na wasanii wa nchi za magaribi wakati unga wa ugali kumudu ni shida,Tunasubiri tuone. Habari Zaidi

'Arusha Times' waiba story ya 'Nation'
Kumbe magazeti huibiana habari?

Ajabu ni kwamba STORY iliandikwa kwanza na Daily NATION, na badala AT waseme waliikopi kutoka Nation, wao wanajifanya kwamba story ni yao, tena wanadai imeandikwa na Staff Reporter wao.Waandishi wa habari wanapoibiana habari, nini hawawezi kuiba? Gazeti la waswahili wanaoandika kiingereza, siyo ajabu wakiamua kuwa majambazi wanaoiba story zilizoandikwa kwa kiingereza sanifu.Kama kizungu kinawapiga chenga, si wawasiliane kwa lugha wanayoijua kuliko kuamua kuwa majambazi wa habari? More

Mark Kariuki alivyowatapeli Wachungaji Nairobi

Juanita Bynum akiwa na mwenyeji wake Mark Kariuki
Baada ya Mkutano uliofurika watu wengi Uhuru Park, Sasa Wachungaji wanalalamika kwamba Mark Kariuki aliwatapeli.Aliwaita kwenye moja ya Hoteli kubwa Nairobi, na kuwalisha chakula cha jioni. Kisha aliwauzia sera zake kuhusu mgeni anaetarajia kumwalika. Aliwataka wachungaji hao kuchangia mkutano huo kipesa kwani angetaka kuwaonyesha Wamarekani kwamba Afrika wanaweza kuudhamini mkutano wa Injili.Wachungaji walikubaliana naye na kuanza kuuchangia mkutano. Ilipofika siku yapili ya Mkutano, wachungaji hawakuyaamini masikio yao pale mgeni wao alipotamka kwamba alituma shilingi milioni nane kuugharamia mkutano huo.Kwa sasa vidole vyote vinaelekezwa kwa Mark Kariuki pamoja na Kanisa la Deliverence Church waliouteka mkutano huo. Umoja bandia, sasa umeishia kulaumiana. Habari Zaidi


Serikali Yajikanyaga

Polisi mjini Nairobi wakionyesha vifaa vipya ambavyo Serikali iliagiza kutoka ngambo ili kuwanasa madereva walevi. Wenyewe Serikali
wameruhusu pombe ziuzwe kila mahali, na sasa wanawasaka madereva walevi. Je itakuwa kuwanasa madereva walevi, au ni kuwaambukiza magonjwa kutumia vyombo hivyo ambavyo vinatumiwa na Polisi wasiozingatia masharti ya afya? Wanaotumia vyombo hivyo, hulazimishwa kupuliza ili kiwango cha pombe miilini mwao kijulikane? huku wengine wakiacha mate yao mahali ambapo lazima kila dereva aweke mdomo wake hapo. Je hiyo ni sawa?

Pirater Mkuu Anaswa

Mwenye koti jekundu ni Mwandishi wa Habari akiwategea sikio wasanii nje ya makao makuu ya Nation Media. Kilio chao ni wizi wa kazi zao. Walidai kwamba wamemnasa mshukiwa ambaye wanadai ndiye mzizi mkubwa wa wizi wa kazi zao za kisanii. Habari Zaidi


Tanzania wabadili pasipoti tena
A country without National IDs, but they keep on changing passports every now and then.
What a SHAME?


Mchungaji Munishi akiwa katika ofisi za ubalozi wa Tanzania jijini Nairobi hivi majuzi. Alikuwepo kuibadili pasipoti yake, kufuatia zoezi la serikali ya Tanzania kuzibadili hati za kusafiria.
Wenye pasi wanatakiwa kuomba upya, na kutimiza masharti yote ikiwa ni pamoja na kulipa shilingi elfu nne za Kenya. Isitoshe kila mwombaji lazima achukuliwe alama za vidole vya mikono yote miwili. Wadadisi wa mambo ya kisiasa wanahoji uhalali wa serikali kubadili pasipoti wakati huu wa uchaguzi. Wengine wanaliona hilo kama mbinu ya serikali ya CCM kutafuta pesa za kuugharamia uchaguzi. Pasipoti ambayo ilikuwa ikigharimu shilingi elfu tano za Tanzania, sasa inagharimu zaidi ya shilingi elfu hamsini za Tanzania. Je mwananchi wa kawaida Tanzania atapata wapi TSHS.50,000? Habari Zaidi



Eti Wanjiru Kahaba?

"BIshop" Magreth Wanjiru Ametangaza rasmi kutounga mkono katiba mpya ambayo Kibaki anataka wakenya waipitishe kwenye kura ya maoni. Magazeti nchini Kenya yameanza kumchambua Mama Magreth Wanjiru huku mengine yakimwita Kahaba. Je kuna ukweli kwenye tuhuma hizo?Habari Zaidi

Gospel Television Moto wa kuotea mbali

Ikiwa ndio kwanza inajitayarisha kurusha matangazo yake, GTV imekuwa tishio kwa Serikali Tanzania. Aliyekuwa Rais wa kimabavu nchini humo William Benjamin Mkapa aliamuru polisi wawatie mbaroni wote watakaopatikana na VCD za GTV. Kisa ni kwamba Gospel Television ilikuwa imezungumzia uwezekano wa Mkapa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kutumia madaraka vibaya. GTV ilikuwa imedai kwamba, Mkapa akiwa madarakani aliwaamuru POLISI wawaue Wazanzibari zaidi ya 70 kwa kosa la kusema CCM Chama Cha Majambazi hawakitaki. Pamoja na mambo mengine GTV ilipendekeza tume ya kumchunguza Mkapa iundwe na akipatikana na makosa sheria ichukue mkondo wake. Pia GTV ilidai kwamba Mkapa aliitawala Tanzania kama mali yake binafsi kwani hakutaka ushauri wa mtu yeyote. Bado msimamo wa GTV ni huo na hatuombi msamaha kwa Mkapa wala CCM. Habari Zaidi
Hotuba ya Munishi kwa TAIFA

Vs

NTV Wavuta viatu badala ya Soksi
Kuboresha NTV Haimaanishi kupora watangazaji kutoka KTN. Badala yake inaonyesha uvivu wa kutengeneza watangazaji wenu, au kuwatafuta wapya.
Baada ya kurupushani na Lucy, sasa Nation wanaonekana kushika adabu. TV yao wanasema itatuwasha badala ya sisi kuiwasha.Wengi wametafsiri hiyo kama ongezeko la vipindi vinavyohusiana na "ngono" Tayari wameanza kuonyesha nyimbo ambazo waimbaji na wachezaji wako nusu uchi kama siyo uchi kabisa. Ikiwa walimaanisha kuiwasha jamii kwa jinsi hiyo, basi wamekosea. Tunatakiwa kulaani vipindi vya ngono kwenye TV. Na Nation wajue hivyo..Habari Zaidi


GOSPELTV WATCH PRO-LIFE VIDEOS


GTV Online

Gospel Television ambayo Studio zake ziko Nairobi Kenya, Sasa itaanza kurusha matangazo yake kutumia Internet. Mipango yote imekamilika na tuko mbioni kukamilisha ile ya kiufundi ili tuwe Online ulimwenguni kote. Endelea kuutupia macho ukurasa huu. Kwa sasa unaweza kuisikia sauti ya GTV. Habari zaidi

Gospel Redio FM
Sasa unaweza kuisikiliza Redio INJILI FM OnLine.
TAHARIRI: Wahubiri Tegemeeni Mungu

Wimbo mpya "Nateseka Natukuza"
"Wanahabari Wanafiki" Wimbo
MASAI: "Hakuna Nuru Gizani" VICHEKESHO
Hotuba ya Munishi kwa TAIFA
"Yesu atakuponya bure" TAHARIRI
Wimbo mpya "Mpende Adui "
GUMZO"Aibu wanahabari!! "


Habari za hapa na pale

Kenedy Ochieng Asema ana UKIMWI Mugabe na Mkapa lao moja
Gospel tape banned by Dar officials Vituko Makanisani Sokoni Gikomba
Munishi Magazetini

Hotuba ya Munishi kwa TAIFA

Kisii yaongoza kwa Injili




Wachungaji na wageni walioudhuria kongamano la kipekee mjini kisii. Habari zaidi

Tuzo la Mwanzo wa Mwisho?

Ester Wahome Mwimbaji wa nyimbo za Injili akipokea tuzo la KISIMA kutoka kampuni ya "Nation" Pamoja nae ni mwimbaji wa nyimbo za dansi Saimoni Kihara maarufu kwa jina la Musaimo. Kwamba makanisa yamewatupa waimbaji wao mpaka kufikia hatua ya kupewa tuzo na watu wasio wa Kanisa tena kwenye vilabu vya usiku, hiyo ni aibu kwa Kanisa pamoja na waimbaji wanaokubali kuidhalilisha Injili. Tuzo la waimbaji wa Injili liko mbinguni. Lakini haya matuzo ya kina "Nation" na mengine ya watu 'Wa Kora", yanawafaa wenyewe. Ndio maana kila mwimbaji wa Injili aliyekubali kupewa tuzo za kidunia, inakuwa huo ndio mwanzo wa mwisho wake. Tunaomba mambo yasiwe hivyo kwa Ester Wahome. Habari Zaidi


50 wafa Ukambani Baada ya kunywa pombe ya sumu


Hawa ni baadhi ya waasiriwa wa pombe hiyo ambayo Serikali inaiita haramu

Takriban watu 50 wamepoteza maisha yao baada ya kunywa pombe inayosadikiwa ilikuwa na kemikali za sumu. Pombe hiyo maarufu kama 'KUMI KUMI' huuzwa shilingi kumi za Kenya. Watu wengi wa kipato cha chini wamekuwa hawana jinsi isipokuwa kuibugia 'KUMI KUMI' baada ya kazi ngumu mchana. Tukio hilo la kushangaza lilitokea Machakos kilomita 50 kutoka jijini Nairobi.Kufuatia tukio hilo Rais Kibaki ameamuru Polisi wasake pombe zote za kienyeji nchi nzima Habari Zaidi

Ajali ya Kutisha

Moja kati ya ajali mbaya Tanzania HABARI ZAIDI
Gazeti la "MWANANCHI" Tanzania lafichua
Tizama video ya Munishi

Umewahi kujiuliza kwa nini mabalozi wa Tanzania nchi za nje karibu wote ni wanajeshi wastaafu? Je Serikali huwatumia kufanya ukachero kwenye nchi hizo? Au hujihusisha na mambo ya kidiplomasia kama yalivyo? Je wanajeshi na wanadiplomasia ni taaluma moja? Kwa nini Serikali zote tangu Nyerere zimekuwa zikifuata desturi hiyo? Je ni mbinu ya kuwatawanya wanajeshi ili wasiweke vichwa pamoja kuitoa serikali dhalimu ya CCM? Hayo na mengine mengi, Mwandishi wetu atayaangalia katika makala haya. Habari zaidi

"Standard" Kenya Latoboa siri


Aibu Yaifunika Tanzania

Serikali ya Mkapa imefanya kosa la kiistoria pale ilipowafukuza waandishi wa habari wa nchi jirani ya Kenya. Waliyataka wenyewe, na yalipokuja sasa wanayakimbia. Baada ya gazeti la "Mwananchi' kuuzwa kwa kampuni ya 'NATION", Wakenya waliwekeza mabilioni ya dola za Kimarekani katika sekta ya habari na utangazaji nchini Tanzania. Kile ambacho hawakukijua, ni kwamba sekta hiyo haijawahi kuwa huru Tanzania. Walipoanza kuandika habari kulingana na taaluma yao, gazeti la 'Mwananchi' lilianza kuchanja mbuga Tanzania, na kuwa moja kati ya magazeti yanayoongoza nchini humo. Serikali ikaliona hilo. Kama kawaida yao kuthibiti habari, walijaribu kulitumia gazeti la 'Mwananchi" liwapigie debe CCM wakati huu wa uchaguzi. Inasemekana wanataaluma hao waliikatalia serikali usoni, jambo lililosababisha kutimuliwa kwao. Mkapa ameithihirishia dunia kile ambacho walikuwa wakikijua tayari. Kwamba Tanzania hakuna uhuru wa kutoa mawazo. Na kwamba utitiri wa vyombo vya habari Tanzania ni kifunga macho ili jumuia ya kimataifa ione kwamba kuna uhuru wa habari, kumbe asilimia 99 ya vyombo hivyo humilikiwa na serikali pamoja na maajenti wake. Inasemekana Mkapa mwenyewe anamiliki zaidi ya magazeti 8 yakiwemo yale ya kidini ambayo hayaachi kuweka picha yake mbele. Anapomaliza urais na kuirudia kazi yake ya uandishi, Mkapa atakumbukwa kama mwanahabari aliyepata madaraka yakamlevya, kisha akaanza kuwatesa wanahabri wenzake.



Serkali ya Tanzania inaongozwa na wahuni. Usipounga mkono maovu yao, basi watakufanya chochote. Watatumia kila chombo cha dola. Idara ya UHAMIAJI ikiwa mojawapo. Ni kawaida yao. Wamezoea. Na hawapelekwi kokote. Kinachoniumiza moyo, ni mabilioni ya shilingi za Kenya "NATION walizotapeliwa na Serikali ya Tanzania. Kwamba sasa wanawatimua, Mtu anaweza jiuliza kwa nini waliwauzia kampuni hiyo ya "MANANCHI" ikiwa kuwapa vibali ni vigumu? Hata kama wewe ni Mtanzania usishangae kuitwa mkimbizi kutoka Zambia. Wana habari wa "NATION" wako Tanzania kufanya kazi kulingana na taaluma yao na siyo kuipigia debe CCM. Kama Mkapa alifikiri kwamba "NATION" ni "UHURU" na "MZALENDO" magazeti ya chama, atakiona kilichomnyima kuku kutoa maziwa anyonyeshe vifaranga. Namshukuru Mungu kwamba "NATION" wamejionea wenyewe yale ambayo nimekuwa nikiyalalamikia kwa miaka mingi. Kanda yangu ilipigwa marufuku kwa kusema "CCM aliyoanzisha Nyerere imezeeka, Sijui "MWANANCHI" walisema nini. Lakini Wahuni wa DAR, wameanza fujo zao. Safari hii wameuma kubwa kuliko uwezo wao kutafuna. Pengine wateme. Wakimeza itawakwama kooni.Jipeni moyo "NATION" Mungu ni mkuu kuliko CCM na Mkapa mwanahabari anaewatesa wanahabari..Habari Zaidi




Zanzibar Kunaashiria Moto

Pastor Pius Kongo Alaumiwa

Pastor Pius Kongo Aliyekuwa TAG Moshi mjini, kabla ya kufungua kanisa lake. Ambalo sasa linamtupia kila aina ya lawama Habari Zaidi

Jihadhari nao ni WASHIAMA!!

Washiama Vijana mashuhuri wa kuimba nyimbo za Injili nchini Kenya
Habari Zaidi

Waislamu wamlalamikia Mwinyi

Aliyekuwa Rais wa awamu ya pili Tanzania Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi Watanzania wanamheshimu kwani yeye ni nyota ya mabadiliko Tanzania. Alikuwa na ujasiri wa kupinga sera za Nyerere akiwa hai, na kuleta mageuzi Tanzania ambayo Mkapa ameyadidimiza matumaini ya Watanzania. Habari Zaidi

"Kikwete Tosha" asema Mchungaji

Mchungaji Paul M.K. Mduma Akiwa katika Ofisi za GTV alielezea masikitiko yake kwamba, vyombo vya habari vimeanza kumchafua Kikwete aliyemjua tangu akiwa mwanafunzi Kibaha Secondary School. Alidai kwamba walisoma wote kwa muda wa miaka minne. Tangu mwaka 1966 hadi 1969 Habari Zaidi

Waruinge Atawazwa Uchungaji

Alikuwa kiongozi wa kundi la Mungiki ambalo Serikali ya Kenya ililiita "kundi haramu" Aliokoka mwaka 2003 na miaka miwili baadaye alitawazwa kuwa Mchungaji Hezekia Ndura Waruinge

Kikosi cha Living Water Kawe

Waimbaji wa kikundi cha Living Water wakiimba nyimbo za kumtukuza Mungu

Komba Ajikomba na CCM

Wanamwita "Kapteni" Komba Msanii anayetumia sanaa yake kuwatukuza wanadamu badala ya Mungu. Sasa anajuta kuwapandisha wanasiasa ngazi huku mwenyewe akibaki chini.Anasema kama siyo yeye Mkapa asingeuona Urais na hatimaye awe tajiri wa kutisha Tanzania. Mkapa alimsahau Komba mara tu alipoingia Ikulu. Mungu anamwita Komba amtumikie. Uzee unapomnyemelea Komba, laiti angeona mwanga amtukuze Mungu badala ya wanasiasa waongo.Kila la Kheri Bwana Komba.

Padre Atuhumiwa kwa UBASHA

Padre Sixtus Kimaro Akiwa mahakamani Kisutu Dar.
Ameshitakiwa kwa tuhuma za kumlawiti mvulana wa miaka 17
Sisi tunasema "Lisemwalo Haliko, Kama liko, Lilikuwepo." HABARI ZAIDI

Simbeye Mchawi Aliyeokoka


Bwana Zebius Mulingwa Simbeye Akiwa na Joyce Wairimu Maina Kericho Kenya


Mtoto apatapo Mtoto


Siri za Kakobe



Askofu Nnko ailalamikia Serikali


Kuishi Amerika ni haki yako


Samples. 6 second of every song

SIDE A

  1. Mpende Adui
  2. Wahariri Watubu
  3. Yesu Bima Tosha
  4. Kuhubiri ni Taluma
  5. Maji Yana Mdudu
  6. Gazeti Siyo Ugali

SIDE B

  1. Yesu Aponya
  2. Jirani Mchokozi
  3. manabi.wav
  4. Rushwa Adui
  5. Msiabudu Amerika
  6. Baba Nakuabudu

SIDE A

  1. Malebo
  2. Usichanganye
  3. Yesu Mambo Yote
  4. Ukimwi Na Maisha
  5. ? Wanamwabudu Nani ?

SIDE B

  1. Yesu Nakupenda
  2. Mageuzi Na Injili
  3. Kazi Na Wanawake
  4. Maombi
  5. Yesu Mwanzo Na Mwisho

SIDE A

  1. Yesu Aliniita
  2. Bwana Nashangaa
  3. Tuonane Milele
  4. Wamwendea Yesu
  5. Msalabani Pa Mwokozi
  6. Yesu Kwetu Ni Rafiki

SIDE B

  1. Bwana Uliyewaita
  2. Kumtegemea Mwokozi
  3. Sioni Haya Kwa Bwana
  4. Yesu Unipendae
  5. Yesu Nakupenda
  6. Ati Tuonane Mtoni

SIDE A

  1. Makosa Ni Kosa
  2. Fikiri Mwanadamu
  3. Dhambi Ni Nini
  4. Yesu Anaokoa

SIDE B

  1. Ajirekebishe
  2. Kaka Ananitesa
  3. Christmas
  4. Anarudi Yesu

SIDE A

  1. Chini Ya Mwamba
  2. Paulo Na Sila
  3. Kifo Mapatano
  4. Nimekukimbilia Nisiaibike
  5. Upendo Ule Wa Kwanza

SIDE B

  1. Salama Rohoni
  2. Hakuna Mungu Kama Wewe
  3. Nimuogope Nani
  4. Huna Cha Kujivunia
  5. Amua Mwenyewe

SIDE A

  1. Ninyime Vyote Niachie Yesu
  2. Maisha Yalitisha
  3. Fashoni Ni Yesu
  4. Anakuita
  5. Waokoe Vijana
  6. Uliyaona Zamani?

SIDE B

  1. Ulimi
  2. Pesa
  3. Dhambi
  4. Siku Za Mwisho
  5. Nielezeje

Twende nikutembeze Nairobi



Siku ya kufa Nyani miti yote huteleza. CCM ni Nyani ambaye siku ya kufa kwake imekaribia. Haijalishi uhodari wa CCM kuparamia miti zaidi ya miaka arobaini, lakini safari hii miti yote inateleza. Watapigiza chini kwa kishindo, na huo ndio utakuwa mwisho wao. Watanzania tunataka ENZI MPYA bila CCM Habari Zaidi

Soma Magazeti ya kila siku Hapa

Nation Media
Nation Kenya


IPPMedia TZ


BCSTIMES TZ


Standard Kenya



Vision Uganda


Monitor Uganda

Matangazo

Study The Bible

Passage (eg. John 3:16):

Search word(s) (eg. saved):


Read Bible



Faustin Munishi Tell. 25472602445 Nairobi Kenya East Africa
E-mail: munishi@munishi.com  |  munishifaustin@yahoo.com

Check mail at Hotmail
Check Mail at Yahoo